LIGI ya Championship ya NBC msimu wa 2025/26 inaendelea kushika kasi huku vita ya ufungaji ikizidi kupamba moto huku wachezaji mbalimbali wakionyesha uwezo wao wa kutikisa nyavu.
Kinara wa orodha hiyo anaekipiga katika kikosi cha Kagera sugar Obrey Chirwa tayari ameweka kambani mabao 14 na kuwa kileleni mwa wafungaji.
Akifuatiwa na Adam Uledi wa Transit Camp ambaye amehamia KMC inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC mwenye mabao 11 sawa na Ramadhani Hashimu kutoka timu ya B19 inayopambana vikali kusalia Ligi ya Championship ya NBC.
Nafasi ya tatu inashikwa na Boniface Brown wa Mbeya Kwanza mwenye mabao 10 sambamba na Abdereheman Mussa wa Transit Camp na Maulid Shaban kutoka Geita Gold wote wakiwa na idadi hiyo ya mabao.
Ushindani huu unaonyesha wazi kuwa msimu huu ni wa ushindani mkubwa ambapo kila mchezaji anapambana kuisaidia timu yake pamoja kuwania kiatu cha ufungaji bora.