‘FEI TOTO’ NA REKODI YA HAT-TRICK YA MAPEMA ZAIDI LIGI KUU YA NBC 2023/2024.

 

MCHEZAJI Feisal Salum ‘Fei Toto’ ameingia kwenye rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga Hat-trick ya haraka zaidi Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 akitumia dakika 9 .

Feisal Salum alifunga Hat-trick hiyo kwenye mchezo wa kwanza Ligi Kuu ya NBC dhidi Kitayosce iliyobadili jina na kuwa Tabora United katika dakika ya tatu, sita na 12 hivyo kutumia dakika tisa kufunga idadi hiyo ya mabao.

Msimu wa 2023/2024 Feisal Salum amehusika kwenye mabao 26 ya kikosi cha Azam akifunga mabao 19 akitoa pasi za mabao 7 na kuwa mchezaji wa Azam aliyehusika kwenye mabao mengi zaidi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *