Ligi ya NBC Championship inazidi kushika kasi ambapo mizunguko tisa imeshachezwa mpaka sasa kwa timu zote 16 zinazoshiriki ligi hiyo ambayo kila timu imeonekana ikipambana kuhakikisha inapanda daraja msimu ujao.
Mtibwa Sugar ndio wanaongoza msimamo wakiwa na alama 20 wakiwa wamefunga mabao 15 na kufungwa manne sambamba na Geita Gold wakiwa na alama 20 huku wakiwa wamefunga mabao 11 na kuruhusu manne.
Timu za TMA,Songea United,Mbeya City na Stand United kila moja imevuna alama 18 huku TMA wakifunga mabao 15 na kuruhusu nane, Songea wamefunga 12 na kuruhusu saba, Mbeya City imefunga mabao 15 ikiruhusu 11 na Stand United imefunga nane ikiruhusu mabao saba.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena Novemba 22 kwa michezo miwili, Transit Camp itakuwa mwenyeji wa Mbeya Kwanza huku timu ya BigMan itaikaribisha Kiluvya kwenye mchezo wa pili.