MTIBWA, TMA, MBEYA CITY WABABE WA MABAO NBC CHAMPIONSHIP.

IKITIMIZA mizunguko tisa tangu kuanza Ligi ya NBC ya Championship inazidi kushika kasi huku timu za Mtibwa Sugar, TMA na Mbeya City zikiongoza kwa kufunga mabao hadi sasa.

Hadi sasa timu hizo zimefanikiwa kufunga mabao 15 huku Mtibwa ikiruhusu mabao manne, TMA ikiruhusu nane na Mbeya City ikiruhusu mabao 11.

Kiluvya iliyopanda daraja kutoka Ligi ya First League ndio timu iliyofunga mabao machache hadi sasa ikifunga manne huku ikiwa timu iliyofungwa mabao mengi (15) na kushika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi ya NBC championship hadi sasa.

Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja kutoka Ligi Kuu ya NBC msimu uliomalizika hadi sasa inashikilia uongozi wa NBC Championship ikiwa na alama 20 sawa na Geita Gold iliyoshuka kutoka Ligi Kuu pia.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *