LIGI namba sita kwa ubora barani Afrika Ligi Kuu ya NBC inarejea Novemba 22 baada ya mapumziko ya kalenda ya FIFA ambapo ijumaa Pamba Jiji ya Mwanza itakuwa mwenyeji wa Simba ya Dar es Salaam.
Pamba wamecheza michezo 11 mpaka sasa huku wakiwa wamevuna alama nane na wakiwa nafasi ya 15 katika msimamo wa Ligi Kuu.
Simba wamecheza michezo 10 wakiwa wamevuna alama 25 na kushika nafasi ya kwanza katika msimamo.
Mchezo huo utachezwa siku ya ijumaa katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza majira ya saa 10 alasiri.