UKISALIA mchezo mmoja pekee Ligi ya Championship ya NBC kutamatika Mchezaji wa Mtibwa Sugar Oscar Masai anashikilia rekodi ya kucheza dakika nyingi zaidi kwenye ligi hiyo hadi sasa.
Oscar amecheza dakika 2627 hadi sasa huku akiwa ameisaidia Mtibwa kurejea kwenye Ligi Kuu ya NBC na endapo timu yake itashinda mchezo wake wa mwisho dhidi ya Kiluvya itakuwa bingwa mpya wa Ligi ya Championship ya NBC.
Andrew William wa Stand United ya Shinyanga anashika nafasi ya pili kwa kucheza dakika nyingi akiwa nazo 2614 huku timu yake ikiwa nafasi ya tatu ya msimamo na ikitarajiwa kuchezo michezo ya mtoano kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26.
Evart Joseph wa African Sports ya Tanga anashika nafasi ya tatu akiwa na dakika 2580 huku timu yake ikishika nafasi ya 15 ikiwa kwenye mstari wa kushuka daraja na endapo African Sports itapoteza mchezo wake wa mwisho dhidi ya Transit Camp nyumbani itakuwa imeshuka daraja rasmi na kushiriki Ligi ya First League msimu wa 2025/26.