JKT KUWAKARIBISHA SIMBA ISAMUHYO LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC itaendelea kesho kwa mchezo mmoja ambapo timu ya JKT Tanzania itaikaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni mkoani Dar es Salaam  majira ya saa kumi jioni.

Mchezo huo ambao ni mchezo wa mzunguko wa 25 ulishindwa kufanyika hapo awali kutokana na ugumu wa ratiba ya Simba iliyokuwa  na michezo ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

JKT Tanzania ipo nafasi ya saba katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imefanikiwa kufunga mabao 24 na kuruhusu mabao 24 katika michezo 26 ambayo timu hiyo imeshacheza mpaka sasa huku ikikusanya alama 32.

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo  wa Ligi  Kuu ya NBC ikiwa imekusanya alama 60 katika michezo 23 ikifunga mabao 54 na kuruhusu mabao tisa .

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *