JKT TANZANIA YATINGA LIGI KUU YA NBC

SARE ya bao moja iliyopata timu ya Pamba kutoka mkoa wa Mwanza dhidi ya Mbuni ya Arusha leo imeihakikishia JKT Tanzania kupanda Ligi Kuu licha ya kupoteza mchezo wake ugenini mbele ya Kitayosce ya Tabora kwa mabao 3-2.

JKT inarudi Ligi Kuu ya NBC ikiwa na michezo mitatu mkononi huku vita ikibaki kwa Kitayosce na Pamba kusaka mmoja wa kuungana na Maafande hao kupanda moja kwa moja bila kucheza hatua ya mtoano.

Iwapo Pamba itashinda mechi zote zilizobaki itafikisha pointi 61 huku Kitayosce nayo ikishinda zote itafikisha alama 62.

Ushindi wa Kitayosce umeiweka nafasi ya pili kwa alama 53, huku Pamba wakishuka Hadi nafasi ya tatu kwa pointi 52 na timu zote zimebakiza mechi tatu kuamua hatma yao.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *