MCHEZO wa Ligi Kuu NBC kati ya Dodoma Jiji dhidi ya KMC umemalizika kwa kushuhudia kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ akianza mchezo wake wa kwanza kama kocha mkuu wa KMC kwa kufungwa bao 1.
Bao la Dodoma Jiji limefungwa dakika ya 19 na mshambuliaji Collins Opare aliefikisha mabao saba na kuendelea kuididimiza KMC nafasi ya 14 ikisalia na alama 26.
Katika mechi 2 za msimu huu walizokutana zote Dodoma Jiji imepata ushindi, mchezo wa mzunguko wa kwanza uliofanyika katika uwanja wa Uhuru, Dar es salaam, Dodoma Jiji waliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Azam FC baada ya kuifunga Mtibwa Sugar 2-1 nyumbani imefanikiwa kushinda mechi ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Ruvu Shooting kwa mabao 3-1 ugenini.
Ruvu Shooting Imeendelea kupoteza matumaini ya kusalia Ligi Kuu msimu ujao baada ya kushinda mechi mbili pekee kati ya 10 mfululizo zilizopita ikikusanya alama 20 katika nafasi ya mwisho kwenye msimamo.