‘KIVUMBI’ CHA LIGI KUU YA NBC KUANZA LEO.

PAZIA la Ligi kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 linafunguliwa rasmi leo Agosti 15 kwa michezo mitatu kuchezwa katika viwanja mbalimbali.

Mchezo wa kwanza wa ufunguzi utazikutanisha Ihefu dhidi ya Geita Gold saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Highland Estate, Mbeya mchezo wa pili utazikutanisha Namungo dhidi ya JKT Tanzania saa 12:30 usiku katika Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa Mkoani Lindi na mchezo wa mwisho ni kati ya Dodoma Jiji na Coastal Union saa 3:00 usiku uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Msimu huu mpya wa Ligi Kuu ya NBC unashirikisha jumla ya timu 16 zitacheza jumla ya michezo 30 ‘kila moja’ uwanja wa nyumbani na ugenini na kufanya jumla ya michezo 240 sawa na michezo 120 nyumbani na 120 ugenini kwa timu zote

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *