SIMBA BINGWA MPYA WA NGAO YA JAMII.

Baada ya timu ya Yanga kutwaa ubingwa wa Ngao ya Jamii kwa miaka miwili mfululizo hatimaye timu ya Simba Leo Agosti 13, 2023 imefanikiwa kushinda mchezo wa fainali na kutwaa ubingwa huo.

Simba wametwaa ubingwa huo kwa kuifunga Yanga Kwa mikwaju ya penati 3-1 ikiwa ni baada ya mchezo huo kumalizika kwa suluhu ndani ya dakika 90.

Golikipa wa Simba Ali Salim ndiye aliyeibuka shujaa wa mchezo baada ya kuokoa penati tatu na kuisaidia timu yake kutwaa ubingwa huo.

Baada ya mchezo huu Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kuanza Agosti 15 kwa michezo kati ya Ihefu na Geita Gold, Namungo na JKT Tanzania, na Dodoma dhidi ya Coastal Union.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *