TIMU ya KMC ya Dar es Salaam imefanikiwa kupata ushindi wa kwanza nyumbani dhidi ya Singida Black Stars kwa mabao 2-0 tangu kurejea kwa Ligi Kuu ya NBC iliyokuwa kwenye mapumziko mafupi.
Mabao mawili yaliyofungwa na Oscar Paulo kipindi cha kwanza yalitosha kuzamisha jahazi la Singida BS ambayo haijapata ushindi tangu kurejea kwa ligi hiyo.
KMC imefanikiwa kupata ushindi baada ya kupoteza mchezo uliopita ugenini dhidi ya Coastal Union kwa mabao 2-1 huku Singida ikilazimishwa sare ya 2-2 mchezo uliopita dhidi ya Kagera Sugar.
KMC imefikisha alama 22 na ‘kukwea’ hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC huku Singida BS ikisalia nafasi ya nne na alama 31.