BAADA ya kupigwa michezo miwili jana Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo kwa michezo minne ya mzunguko wa 28 katika viwanja vinne tofauti .
Mchezo wa kwanza utapigwa majira ya saa 8:00 mchana katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni Dar es Salaam ambapo JKT Tanzania itaikaribisha timu ya Fountain Gate kutoka Manyara.
Saa 10:00 alasiri itapigwa michezo miwili ambapo mchezo wa kwanza ni kati ya Young Africans ikiwaalika Namungo katika uwanja wa KMC Complex mkoani Dar es Salaam na KenGold itaikaribisha Pamba Jiji katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Mchezo wa mwisho utachezwa saa 1:00 usiku ambapo timu ya Azam itakuwa mwenyeji wa timu ya Dodoma Jiji katika uwanja wa Azam Complex, Dar.