KAGERA SUGAR ‘HATIHATI’ KUSHIRIKI LIGI KUU YA NBC MSIMU UJAO.

MATUMAINI ya wapenzi na mashabiki wa timu ya Kagera Sugar kusalia Ligi Kuu ya NBC yamezidi kufifia baada ya kufungwa na timu ya Mashujaa katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera jana kwa bao 1-0.

Timu hiyo imeshacheza michezo 28 ya Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/25 na kufanikiwa kuvuna alama 22 ikifunga mabao 22 na kuruhusu mabao 40 huku ikiwa imebakisha michezo miwili kumaliza msimu.

Aidha timu hiyo endapo ikishinda michezo yote iliyobakia itaweza kufikisha alama 28 ikiwa ni tofauti ya alama moja na Pamba Jiji ambayo ina alama 27 ikifunga mabao 18 na kufungwa mabao 32 huku ikiwa imebaki michezo mitatu mkononi.

Endapo Pamba Jiji itashinda mchezo wa leo dhidi ya KenGold rasmi Kagera Sugar itashuka daraja na kushiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *