LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo miwili baada ya kusimama kwa takribani siku 13 kupisha michezo ya kimataifa.
Mchezo wa kwanza utachezwa saa 8:00 mchana kati ya timu ya Tabora United itakayokuwa nyumbani kuikaribisha Kagera Sugar kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora ukiwa mchezo wa kwanza wa Tabora kwenye uwanja wa nyumbani.
Mchezo wa mwisho utapigwa saa 10:15 alasiri kati ya Fountain Gate na KenGold kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo mkoani Manyara wilaya ya Babati.
Huu ni mchezo wa kwanza kwa timu ya Fountain kucheza nyumbani ukiwa pia mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC kuchezwa mkoani Manyara kwenye wilaya ya Babati.