LIGI Kuu ya NBC inarejea leo kwa michezo mitatu itakayochezwa Dar es Salaam, Arusha na Tanga baada ya mapumziko ya takribani wiki mbili kupisha michezo ya kalenda ya FIFA.
Michezo miwili ya kwanza itapigwa majira ya saa kumi jioni mkoani Arusha kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo timu ya Fountain Gate iliyopo nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itaikaribisha timu ya Azam iliyopo nafasi ya tatu kwenye msimamo.
Mchezo mwingine utakaopigwa muda huo ni kati ya Coastal Union iliyopo nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itakuwa mwenyeji wa timu ya Namungo iliyopo nafasi ya 13 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mchezo wa mwisho utakuwa jijini Dar es Salaam ambapo KMC iliyopo nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Lgi Kuu ya NBC itaikaribisha timu ya TRA katika uwanja wa KMC Complex majira ya saa mbili usiku ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kukamilisha siku.