MBEYA KWANZA, MBUNI ZAPETA NBC CHAMPIONSHIP.

TIMU za Mbeya Kwanza na Mbuni zimecheza michezo minne ya Ligi ya NBC Championship bila kupoteza baada ya kila moja kupata ushindi leo.

Mbeya Kwanza inayotumia uwanja wa Nangwanda Sijaona imeifunga Kengold ya Mbeya kwa bao moja kwenye mchezo uliochezwa mapema saa 8:00 mchana.

Mbuni imepata ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya Cosmopolitan kwenye uwanja wa Uhuru na kuifanya Cosmo iliyotwaa ubingwa wa First League msimu uliopita kucheza michezo minne bila kupata ushindi.

Mbeya Kwanza imepanda mpaka nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi ya NBC Championship ikifikisha alama 10 sawa na Mbuni huki Mbeya Kwanza akiongoza kwa tofauti ya mabao mawili.

Mchezo mwingine ulipigwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kushuhudiwa Ruvu Shooting ikifungwa bao moja na Mbeya City na kuifanya Ruvu kuwa timu pekee ambayo haijapata alama msimu huu ikifungwa michezo yote na kushika nafasi ya 16 katika msimamo wa ligi hiyo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *