MBIVU NA MBICHI KUJULIKANA LEO FIRST LEAGUE.

 

JUMLA ya michezo Saba ya First League kundi A na B itapigwa leo Machi 31, 2024 kuhitimisha ratiba ya First League awamu ya kwanza msimu wa 2023/2024.

Kundi A timu za African Sports, Kiluvya, Nyumbu na Malimao tayari zimefuzu kwenda kwenye hatua ya nane bora huku mvutano ukisalia kwenye timu itakayobaki First League msimu wa 2024/2025 kati ya timu zitakazo cheza mtoano wa kushuka daraja timu hizo zikiwa ni Tunduru Korosho, Dar City na African Lyon.

Kundi B mpaka sasa hakuna timu yoyote iliyofanikiwa kutinga hatua ya nane bora (Top 8) huku timu tano pekee zikiwa na nafasi ya kufanya hivyo, Timu hizo ni TRA, Mapinduzi, Rhino Rangers, Tanesco na Mwadui zikiwa timu nne pekee kutoka kundi hili zenye nafasi ya kufuzu hatua ya nane bora .

Timu za Alliance na Kurugenzi zitacheza hatua ya mtoano wa kushuka daraja huku timu ya Kasulu ikiwa tayari imeshashuka daraja.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *