TUKUTANE FIRST LEAGUE NANE BORA.

 

HATUA ya kwanza ya Ligi ya First League iliyokuwa na jumla ya timu 16 kwenye makundi mawili ya timu nane imemalizika jana Machi 31 na kupata jumla ya timu nane zitakazokwenda kutafuta washindi wa kwenda ligi ya NBC Championship .

Timu zilizofanikiwa kuingia hatua hiyo ni African Sports, Kiluvya, Nyumbu na Malimao kutoka kundi A wakati timu za Mapinduzi, Rhino Rangers, Tanesco na Mwadui zikifuzu kutoka kundi B.

Timu za Tunduru kutoka kundi A na TRA kutoka kundi B zimejihakikishia nafasi ya kubakia First League msimu ujao kwa kushika nafasi ya tano kwenye makundi yao.

Timu zitakazocheza mtoano wa kushuka daraja (Relegation Play off) ni Dar City na African Lyon kutoka kundi A huku Kundi B ikikiwakilishwa na Alliance na Kurugenzi.

Timu zilizoshuka Daraja ni Lipuli ya Iringa iliyokuwa kundi A na Kasulu United ya Kigoma iliyokuwa Kundi B.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *