MTIBWA HAIKAMATIKI,JKT YAREJEA KILELENI LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa michezo miwili iliyochezwa mkoani Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri na jiji Dar es saalam katika uwanja wa Mej. Jen Isamuhyo.

Mchezo wa Kwanza uliopigwa saa kumi alasiri kati ya Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons na kushuhudia Mtibwa sugar ikiibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons.

Tanzania Prisons walitangulia kupata bao la mapema dakika ya nane kupitia kwa George Mpole akitumia mkwaju wa penati na Mtibwa sugar ilijibu mapigo kwa kusawazisha dakika ya 38 kupitia Magata Fredrick naye kwa mkwaju wa penati na dakika ya 87 Ismail Mhesa aliipatia Mtibwa bao la ushindi na kuwahakikishia alama tatu muhimu nyumbani.

Katika mchezo mwingine uliochezwa saa moja jioni maafande wa JKT Tanzania waliibuka na ushindi mnono wa Mabao 3-0 dhidi ya Pamba jiji ya Mwanza.

JKT walifungua ukurasa wa mabao dakika ya 34 kupitia kwa Valentino Mashaka bao lililowapa morali na kuwadhibiti Pamba jiji waliojaribu kujibu mashambulizi lakini walishindwa kusawazisha hadi kipindi cha kwanza kinatamatika.

Kipindi cha pili Salehe Karabaka aliendelea kuzamisha jahazi la Pamba jiji baada ya kufunga bao la pili dakika ya 55 na dakika ya 70 Valentino Mashaka aliyewapatia bao la tatu na kuihakikishia ushindi JKT.

Matokeo ya michezo hii yanaendelea kuongeza moto wa ushindani kwenye Ligi Kuu ya NBC huku JKT Tanzania wakiwa kileleni kwa alama 24 na Mtibwa Sugar ikishika nafasi ya tatu baada ya kukusanya alama 20.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *