TCHAKEI MCHEZAJI BORA OKTOBA, TAOUSSI AWABWAGA MOALLIN NA KITAMBI.

Mshambuliaji wa Singida Black Stars Marouf Tchakei amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba wa Ligi Kuu ya NBC huku Kocha wa Azam Rachid Taoussi akichaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi huo.

Tchakei amewashinda Lusajo Mwaikenda wa Azam na Pacome Zouzoua wa Yanga alioingia nao fainali za tuzo hizo baada ya kufunga mabao 3 na kutoa pasi ya mwisho moja katika dakika 360 alizocheza ndani ya mwezi huo.

Singida imeshinda dhidi ya Mashujaa 1-0, Namungo 2-0,Fountain Gate 2-0 na kufungwa 1-0 katika mchezo wao dhidhi ya Yanga.

Aidha Kocha wa Azam Rachid Taoussi amefanikiwa kuwa kocha Bora wa mwezi huo baada ya kuwashinda Abdulhamid Moallin wa KMC na Denis Kitambi wa Singida Black Stars baada ya kushinda michezo mitatu ambayo timu yake ilicheza ndani ya mwezi huo.

Azam walishinda dhidi ya Namungo 1-0, Tanzania Prisons 2-0 na KenGold 4-1 hivyo kupanda kutoka nafasi ya tano hadi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.

Kamati ya Tuzo pia imemchagua Meneja wa Uwanja wa Tanzanite Kwaraa Godwin Israel kuwa Meneja bora kutokana na usimamizi mzuri wa matukio ya michezo na masuala ya miundombinu.

Kwa upande wa Ligi ya NBC Championship kamati imemchagua mchezaji wa Geita Gold Andrew Simchimba kuwa mchezaji bora wa Ligi hiyo baada ya kufunga mabao manne na kutoa pasi ya mwisho moja akiwashinda Adam Oseja wa Geita Gold na Jaffar Maneno wa TMA alioingia nao fainali.

Naye Kocha wa Geita Gold, Amani Josiah amechaguliwa kuwa kocha bora wa ligi hiyo kwa mwezi oktoba ambapo aliiongoza timu yake kushinda michezo minne na kufanikiwa kupanda kutoka nafasi ya tisa mpaka ya kwanza katika msimamo wa ligi hiyo.Bonyeza kiuganishi hapa chini kuona video hiyo WASHINDI WA TUZO ZA MWEZI OKTOBA LIGI KUU YA NBC NA LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *