PAZIA la Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 limefungwa rasmi jana katika mchezo wa dabi ya Kariakoo ambapo timu ya Young Africans iliibuka na ushindi.
Katika mchezo ulichezwa majira ya saa kumi na moja jioni uwanja wa Benjamin Mkapa timu ya Yanga iliifunga timu ya Simba mabao 2-0 yaliyofungwa na wachezaji Pacome Zouzoa na Clement Mzize kipindi cha pili cha mchezo huo.
Mara baada ya mchezo huo Young Africa ilikabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 na kuweka historia ya kulibeba kombe hilo mara 31 huku timu hiyo ikikusanya alama 82 na mtani wao Simba akibaki nafasi ya pili na alama 78.
timu zote zimekata tiketi kushiriki Ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF Champions League) kwa msimu wa 2025/2025 huku Azam na Singida Black Stars wakishiriki Kombe la Shirikisho(CAF Confederation Cup)