NYAVU ZAO HAZIGUSWI NBC CHAMPIONSHIP.

 

MABAO 519 yamefungwa mpaka sasa kwenye mizunguko 27 sawa na michezo 216 ya Ligi ya NBC Championship msimu huu.

Mlinda mlango wa Ken Gold Castor Mhagama anaongoza kwa kucheza michezo mingi bila kuruhusu bao akifanya hivyo kwenye michezo 16.

Mlinda mlango wa TMA Yusuf Abdul anafuatia akicheza michezo 15 bila kuruhusu bao lolote huku Robert Mapigano wa Biashara United akiwa na michezo 10 bila kuruhusu bao .

Jeremia Kisubi wa Mbeya City na Rahim Sheikh wa Mbeya Kwanza wanafuatia kila mmoja akiwa na michezo nane bila kuruhusu bao.

Ruvu Shooting ndio timu iliyo ruhusu mabao mengi ikiruhusu jumla ya mabao 57 kwenye michezo 27 iliyocheza mpaka sasa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *