PAMBA JIJI YAONJA RAHA YA USHINDI, SIMBA, KMC HAPATOSHI LEO.

Ligi Kuu ya NBC jana iliendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa katika Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara ambapo Fountain Gate waliwakaribisha timu ya Pamba Jiji kutoka Mwanza.

Iliwachukua dakika 28 Fountain Gate kufungua ukurasa wa mabao kupitia mchezaji wake Ellie Makono ambapo dakika ya 34 Pamba Jiji waliweka mzani sawa kwa kupata bao kupitia mchezaji wake James Mwashinga kabla ya kuongeza bao la pili katika dakika ya 45 ya mchezo huo kupitia mchezaji Salehe Masoud hivyo kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kushambuliana na dakika ya 85 ya mchezo huo mchezaji Ally Ramadhan aliiongezea Pamba Jiji bao la 3 hivyo kuifanya timu hiyo kupata ushindi wao wa kwanza tangu kupanda Ligi kuu ya NBC huku wakiwa wamecheza michezo 11.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea leo mkoani Dar es Salaam ambapo timu ya Simba itakuwa mwenyeji wa KMC katika Uwanja wa KMC Complex, uliopo Mwenge majira ya alasiri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *