SIMBA, AZAM TIMU ZILIZORUHUSU MABAO MACHACHE LIGI KUU NBC

Ligi Kuu ya NBC inaendelea kushika kasi ambapo mpaka sasa mizunguko 9, 10 na 11 kwa baadhi ya tmu imeshachezwa.

Timu za Simba na Azam ndio timu pekee zilizoruhusu mabao machache mpaka sasa ambapo kila moja imeruhusu mabao matatu tu.

Simba imeruhusu mabao hayo katika michezo miwili dhidi ya Yanga ikifungwa goli moja na mchezo dhidi ya Coastal Union ambapo ilitoka sare ya bao 2-2.

Kwa upande wa timu ya Azam imeruhusu mabao hayo matatu kwenye michezo miwili dhidi ya KenGold ambapo iliruhusu bao moja huku mchezo ukiisha kwa Azam kushinda 4-1 na mchezo dhidi ya Simba ambapo ilifungwa mabao 2-0.

Yanga na Singida Black Stars ndio wanafuatia kuruhusu mabao machache ambapo mpaka sasa wameruhusu mabao manne tu kwenye Ligi Kuu ya NBC.

Yanga imeruhusu mabao hayo baada ya kufungwa na Azam bao moja lililofungwa na mchezaji Gibril Sillah kisha kufungwa na timu ya Tabora United 1-3.

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *