SIMBA YATINGA FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI.

Simba imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga Singida FG kwa mikwaju ya penati 3-2 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Singida ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 11 ya mchezo likifungwa na mchezaji Elvis Rupia huku bao la kusawazisha la Simba likifungwa na mchezaji Fabrice Ngoma dakika ya 90+8.

Simba itakutana na Mlandege ambao ndiyo mabingwa watetezi wa kombe hilo katika hatua ya fainali itakayochezwa januari 13 katika dimba la New Amaan Complex.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *