MCHEZO wa pili wa hatua ya mtoano kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Fountain Gate unatarajiwa kupigwa leo kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya kutafuta timu itakayosalia kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026.
Huu ni mchezo wa mwisho kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC kukutana msimu huu baada ya kumaliza kwenye nafasi ya 13 na 14 ya msimamo zikiwa nafasi za kucheza michezo ya mtoano.
Mchezo huo wa mkondo wa pili utachezwa leo majira ya saa 10:00 alasiri ambapo mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara ulimalizika kwa sare ya 1-1.
Mshindi wa mchezo wa leo atakuwa amekata tiketi ya kusalia katika Ligi Kuu ya NBC huku atakayeshindwa atacheza mchezo wa mtoano dhidi ya timu ya Stand United inayoshiriki Ligi ya Championship ya NBC.