Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

NI VITA YA NANI KUBAKI LIGI KUU YA NBC SOKOINE LEO.

MCHEZO wa pili wa hatua ya mtoano kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Fountain Gate unatarajiwa kupigwa leo kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya kutafuta timu itakayosalia kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026.

Huu ni mchezo wa mwisho kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC kukutana msimu huu baada ya kumaliza kwenye nafasi ya 13 na 14 ya msimamo zikiwa nafasi za kucheza michezo ya mtoano.

Mchezo huo wa mkondo wa pili utachezwa leo majira ya saa 10:00 alasiri ambapo mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara ulimalizika kwa sare ya 1-1.

Mshindi wa mchezo wa leo atakuwa amekata tiketi ya kusalia katika Ligi Kuu ya NBC huku atakayeshindwa atacheza mchezo wa mtoano dhidi ya timu ya Stand United inayoshiriki Ligi ya Championship ya NBC.

YOUNG AFRICANS MABINGWA LIGI KUU YA NBC 2024/2025

PAZIA la Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 limefungwa rasmi jana katika mchezo wa dabi ya Kariakoo ambapo timu ya Young Africans iliibuka na ushindi.

Katika mchezo ulichezwa majira ya saa kumi na moja jioni uwanja wa Benjamin Mkapa timu ya Yanga iliifunga timu ya Simba mabao 2-0 yaliyofungwa na wachezaji Pacome Zouzoa na Clement Mzize kipindi cha pili cha mchezo huo.

Mara baada ya mchezo huo Young Africa ilikabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 na kuweka historia ya kulibeba kombe hilo mara 31 huku timu hiyo ikikusanya alama 82 na mtani wao Simba akibaki nafasi ya pili na alama 78.

timu zote zimekata tiketi kushiriki Ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF Champions League) kwa msimu wa 2025/2025 huku Azam na Singida Black Stars wakishiriki Kombe la Shirikisho(CAF Confederation Cup)

‘PILATO’ WA DABI YA KARIAKOO HUYU HAPA.

RAIA wa Misri Amin Mohamed Amin ndiye atakayechezesha mchezo wa Young Africans dhidi ya Simba maarufu kama ‘Kariakoo Dabi’ Juni 25 kwenye uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Ikiwa Yanga itashinda mchezo huo au kutoa sare ya aina yoyote itaibuka mshindi wa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 na ikiwa Simba itafanikiwa kushinda itaibuka mabingwa wapya wa kombe hilo.

Amin atasaidiwa na Mahmoud El Regal,Samir Gamal Mohamed na Ahmed Mahrous Elghandour wote kutoka nchini Misri huku mtathimini waamuzi akiwa ni Alli Mohamed kutoka nchini Somalia.

Hii ni mara ya kwanza kwa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kusimamiwa na waamuzi wa mchezo kutoka nje ya Tanzania.

Mchezo huo ambao mwenyeji ni timu ya Young Africans yenye alama 79 huku ikiwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Simba yenye alama 78 ikishika nafasi ya pili utapigwa saa kumi na moja jioni.

AZAM YALIPA KISASI KWA TABORA LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Azam imeshusha kipigo kizito cha mabao 5-0 kwa timu ya Tabora United na kulipa kisasi cha kufungwa 2-1 na timu hiyo kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza.

Dakika 11 zilimtosha Abdul Suleiman ‘Sopu’ kufungua ukurasa wa mabao kwa timu yake huku winga wa timu hiyo Gibril Sillah akiiongezea timu yake mabao mawili dakika ya 16 na 29 na dakika ya mwisho ya kipindi cha kwa Iddy Nado aliongeza jingine hivyo Azam Kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 4-0.

Kipindi cha pili Tabora walionyesha nia ya kutafuta bao kwa mashambulizi kadhaa kabla ya ndoto yao ‘kudidimizwa’ dakika ya 89 na mshambuliaji wa Azam Nassor Saadun ambaye aliongeza bao kwa timu yake na kufanya mchezo huo kutamatika kwa mabao 5-0.

Mabao mawili ya Gibril Sillah aliyeibuka mchezaji bora wa mchezo huo yanamfanya kufikisha jumla ya mabao 11 sawa na Pacome Zouzoua wa Young Africans kwenye msimamo wa vinara wa mabao.

SIMBA ‘YAIBAMIZA’ KENGOLD LIGI KUU YA NBC

TIMU ya KenGold imeshindwa kutamba nyumbani kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora baada ya kufungwa na timu ya Simba mabao 0-5 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.

Ilimchukua dakika 20 mchezaji wa Simba Kibu Denis kufungua ukurasa wa mabao huku Ellie Mpanzu akiongeza bao la pili dakika ya 22 ya mchezo huo na dakika ya 25 Kibu Denis alirejea tena nyavuni kuongeza bao la tatu kwa timu yake na kuifanya kuwa mbele kwa mabao matatu.

Dakika ya 36 ya mshambuliaji wa Simba Leonel Ateba aliiongezea timu yake bao la nne na kufanya mchezo huo Kwenda mapumziko ubao ukisomeka 0-4.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu ya KenGold kujaribu kusaka mabao ili kuweka mzani sawa lakini dakika ya 75 mchezaji wa Simba Jean Ahoua aliongeza bao kwa timu yake hivyo mchezo kutamatika kwa ubao kusomeka 0-5.

Kibu Dennis aliibuka mchezaji bora wa mchezo huo huku Jean Ahoua akiongeza wigo wa mabao akifikisha bao la 16 msimu huu na kuendelea kushikilia usukani wa vinara mabao.