YANGA KUWAVAA APR ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI LEO.

 

KOMBE la Mapinduzi linaendelea leo Januari 7 katika hatua ya Robo fainali ambapo mwakilishi wa Ligi Kuu ya NBC Yanga atakuwa kibaruani saa 2:15 usiku kwenye uwanja wa New Amaan Complex kuwakabili APR ya Rwanda.

Yanga wamefika hatua hii baada ya kuongoza kundi C kwa kujikusanyia alama saba kwenye michezo mitatu huku APR wakipita kama best looser kutoka kundi B.

Wawakilishi wengine wa Ligi Kuu ya NBC Azam, Singida na Simba wao watacheza michezo yao ya robo fainali kesho januari 8.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *