TRANSIT YASHINDWA KUIZUIA STAND NBC CHAMPONSHIP.

LIGI ya NBC ya Championship imeendelea kwa mchezo mmoja uliopigwa uwanja wa Mabatini, Pwani kati ya Transit Camp ya Dar iliyochezea ‘kichapo’ cha mabao 3-0 kutoka kwa Stand United ya Shinyanga.

Mchezo ulianza kwa timu zote kushambuliana kwa zamu huku Stand ikitangulia kupata bao mapema lililoipa uongozi hadi kipindi cha kwanza kwanza kinamalizika likifungwa kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Kigi Makasi.

Kipindi cha pili Stand ilijihakikishia ushindi kwa mabao mawili yaliyofungwa na Seleman Seif na Omar Issa na kuifanya Stand kumaliza mchezo huo kwa kukusanya alama zote tatu na bila kuruhusu wavu wao kuguswa.

Matokeo hayo yanaifanya Stand kupaa hadi nafasi ya nne ya msimamo wa ligi ya NBC ya Championship baada ya kukusanya jumla ya alama 35 nyuma ya vinara Mtibwa Sugar wanaoshikilia usukani wa ligi hiyo wakifuatiwa na Geita Gold na Mbeya City.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *