LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja ulioikutanisha timu ya JKT Tanzania na timu ya Simba katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo majira ya saa kumi jioni ulioshuhudia Simba ikishinda kwa bao moja.
Iliwachukua dakika 45 Simba kuandika bao kupitia kwa kiungo wake Fabrice Ngoma baada ya kupokea pasi kutoka kwa mshambuliaji Steven Mukwala na kuifanya Simba kwenda mapumziko ikiwa inaongoza bao moja.
Kipindi cha pili kilianza ambapo JKT Tanzania walijitahidi kulisaka lango la Simba bila kupata bao na hadi mchezo unatamatika ‘Mnyama’ alikuwa mbele kwa bao la Ngoma.
Simba ilifanikiwa kubeba alama zote tatu na kufikisha alama 63 katika michezo 25 iliyocheza huku ikiendelea kusalia katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC