RATIBA YA NBC CHAMPIONSHIP YATANGAZWA.

 

RATIBA ya Ligi ya NBC Championship imetangazwa leo Septemba 9, na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ikitarajiwa kuanza Septemba 20, 2024.

Mechi za ufunguzi zitawakutanisha Mbeya City dhidi ya Bigman FC katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya saa 10:00 alasiri huku mchezo wa pili ukizikutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya Green Warriors saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Manungu mkoani Morogoro.

Ligi ya NBC Championship inajumuisha jumla ya timu 16 ambazo zitacheza michezo 30 ya nyumbani na ugenini hivyo kufanya ligi hiyo kuwa na jumla ya michezo 240.

Kusoma na kupakua ratiba nzima bonyeza kiunganishi hapa chini.

RATIBA-YA-NBC-CHAMPIONSHIP-2024-2025

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *