TIMU ya Simba imeipa maumivu timu ya Tanzania Prisons baada ya kuifunga mabao 0-2 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Mchezo huo uliokuwa muhimu kwa timu zote ambapo Prisons ikitafuta nafasi ya kujitoka katika eneo la hatari huku Simba ikiwa katika harakati za kujiimarisha na kusogea juu zaidi kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Dakika 19 zilimtosha mshambuliaji wa Simba Seleman Mwalimu kufungua ukurasa wa mabao wa mchezo huo huku beki wa timu hiyo Rushine De Reuck akifunga bao la pili dakika ya 45 ya mchezo huo kwa mkwaju wa penati hivyo Simba kwenda mapumziko ikiongoza 0-2.
Kipindi cha pili timu ya Prisons iliamua kucheza kwa kujilinda zaidi ili kutokuruhusu mabao mengine jambo ambalo lilifanikiwa na kwa upande wa Simba wakilinda ushindi wao na kuhakikisha pia wanaondoka na hati safi ambapo pia walifanilisha adhma yao.
Dakika 90 za mchezo huo zilifika tamati na beki wa Simba Rushine De Reuck alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo akiisaidia timu yake kubeba alama zote 3.




