Author: Loveness Bernard

LIGI KUU YA NBC

LIGI KUU YA NBC KUCHEZWA VIWANJA VINNE LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea kwa mzunguko wa 17 huku mechi nne zikichezwa katika viwanja mbalimbali nchini kuanzia majira ya saa nane mchana.

Mchezo wa kwanza utachezwa saa nane mchana katika  uwanja wa Jamhuri Dodoma ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza .

Sambamba na mchezo huo Tanzania Prisons “wajelajela” watawakaribisha timu ya Mashujaa “Wana mapigo na mwendo” katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya  muda ikiwa ni saa nane mchana.

Mchezo  wa tatu  kwa siku ya leo ni timu ya Fountain Gate watawakaribisha  timu ya Simba katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo Babati Mkoani Manyara saa kumi alasiri.

Mkoani Dar es Salaam wenyeji wa  uwanja wa Chamazi  timu ya Azam watawakaribisha timu ya KMC “Kinoboys” katika mchezo utakaochezwa saa moja jioni.

 

MZIZE,DUBE HAWASHIKIKI LIGI KUU NBC

WASHAMBULIAJI wa Yanga Prince Dube na Clement Mzize wameongeza kasi katika mbio za ufungaji bora baada ya kufung mabao mawili kila mmoja katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya KenGold mchezo uliochezwa leo katika uwanja wa KMC.

Licha ya Kocha Mkuu wa Yanga Saed Ramovic kuaga jana ikiwa ni saa chache kuelekea mechi yao dhidi ya KenGold Yanga imefanikiwa kufunga mabao 6-1 .

Prince Dube ndio alifungua ukurasa wa mabao ikiwa ni dakika ya pili ya mchezo huo kabla ya Mzize  kufunga baola pili dakika ya sita ya mchezo huo huku Pacome Zouzuoa akiongeza bao la tatu dakika ya 39 dakika  nne mbele Mzize alirudi tena na kufunga bao la nne huku Dube akiongeza bao la tano dakika ya 43 y mchezo huo na kuwafanya Yanga kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 5-0.

Kipindi cha pili kilianza huku Yanga wakionekana kuzidi kulisakama lango la kenGold  licha ya timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji  ambapo Yanga dakika ya 85 Duke Abuya aliongeza bao la 6 kwa  timu yake.

KenGold walipata bao la kujifutia machozi kupitia mchezaji wake Seleman Rashid baada ya kupiga mpira mrefu ambao ulimshinda kipa wa Yanga Djigui Diarra hivyo mchezo kutamatika kwa 6-1.

Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mchezo huo.

Ligi Kuu itaendelea kesho kwa michezo minne ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba,Tanzania Prisons dhidi ya Mashujaa,Fountain Gate wakiwakaribisha Simba na Azam watacheza na KMC .

CHIKOLA AWALIZA NAMUNGO LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo mkoani Tabora kwa mchezo uliozikutanisha  timu ya Tabora United dhidi ya  timu ya Namungo  katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Mchezo huo uliochezwa majira ya saa nane mchana  ulianza kwa kasi tangu mwanzo kwani dakika ya nne ya mchezo huo mchezaji wa Namungo, Jacob Massawe aliweka mpira wavuni mwa Tabora United.

Offen Chikola ndio alirejesha matumaini ya Tabora United katika dakika ya 32 ya mchezo huo ambapo alifunga bao na hivyo kuifanya mechi kwenda mapumziko wakiwa sare ya 1-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo dakika ya 52 mshambuliaji wa Tabora Heritier Makambo aliiongezea bao la pili timu yake na kufanya ubao kusomeka 2-1 pasi ya mwisho ikiwa imetolewa na Offen Chikola.

Mchezo ulitamatika kwa timu ya Tabora kubeba alama zote tatu mhimu za mchezo huo na mchezaji wao Offen Chikola akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.

SIMBA WAENDELEZA UBABE DHIDI YA TABORA UNITED

Ligi Kuu ya NBC  ambayo ni Ligi ya nne kwa ubora barani Afrika imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United waliwakaribisha Simba katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Mchezo huo umeanza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kucheza kwa tahadhari kwani mchezo huo ulitawaliwa na tambo za Tabora kuwafunga Azam uwanja wa Ali Hassan Mwinyi  na Yanga katika uwanja wa Azam Complex.

Dakika 12 ziliwatosha Simba kufungua akaunti ya mabao kupitia  mshambuliaji wao Leonel Ateba kisha dakika ya 34 kuongeza bao la pili kupitia mkwaju wa penati hivyo kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili .

Kipindi cha pili Simba walizidi kulisakama lango laTabora  licha ya timu hiyo kufanya mabadiliko kwa  wachezaji wawili  lakini Simba walikuwa wakicheza kwa kasi na ufundi mwingi dakika ya 67 beki wa Simba Shomari Kapombe aliongeza bao kwa timu yake akipokea pasi kutoka kwa Leonel Ateba  akififisha matumaini ya Tabora United kurejesha mabao hao.

Dakika 90 za mchezo huo zimetamatika kwa Simba kuendekeza ubabe  kwani tangu Tabora United wapande daraja hawajawahi kuwafungana leo wakiondoka na mabao matatu huku mchezaji  Leonel Ateba akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Simba wamerejea kileleni wakiwa wamefikisha alama 43 wakifunga mabao 34 huku wakiruhusu mabao matano katika michezo 16 ya Ligi Kuu ya NBC waliyocheza .

LADHA ZA LIGI KUU NBC ZAREJEA YANGA WAKIWALIZA KAGERA SUGAR

Ladha za Ligi Kuu ya NBC zimerejea rasmi leo Februari 1 kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam ambapo timu ya Yanga waliwakaribisha Kagera Sugar.

Mchezo ulianza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kushambuliana kwa kasi huku Yanga wakionekana kuutawala mchezo.

Ilimchukua dakika 32 mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize kufungua akaunti ya mabao na kuifanya timu yake kwenda kifua mbele mapumziko licha ya kiungo wa timu hiyo Aziz Ki kushindwa kufunga mkwaju wa penati waliopata timu yake.

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya 60 Mudathir Yahya aliongeza bao la pili kwa Yanga huku wakionekana kuzidi kulisaka lango la mpinzani wao na kutaka mabao zaidi.

Pacome Zouzoua aliongeza bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Kagera Sugar kumfanyia madhambi Max Nzengeli  kabla ya Kennedy Musonda kufunga bao la nne hivyo Yanga kufikisha alama 42 wakiwa wamefunga mabao 36 na wakiruhusu 6.Mchezaji wa Yanga Max Nzegeli amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Ladha za Ligi Kuu ya  NBC zitaendelea kesho mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United watawakaribisha Simba saa kumi alasiri katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.