Author: Loveness Bernard

YOUNG AFRICANS HAIKAMATIKI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Young Africans imefanikiwa kuifunga timu ya Namungo bao moja kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa kwenye uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.

Mchezo ulianza kwa timu zote kushambuliana kwa kasi kubwa kuhakikisha wanachukua alama tatu za Ligi Kuu ya NBC ili kujiweka katika nafasi nzuri kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu.

Dakika 26 zilimtosha mshambuliaji wa Young Africans Laurindo Dilson kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati baada ya mchezaji wao Max Nzengeli kufanyiwa madhambi na mchezaji wa Namungo bao lililodumu hadi mwisho wa kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili timu zote zilirejea kwa kasi kubwa Namungo ikijaribu kufanya mashambulizi ya mbali ambayo hata hivyo hayakuweza kuzaa matunda hadi dakika 90 za mchezo huo zinatamatika wageni Young Africans walifanikiwa kubeba alama zote tatu kutoka kwa Namungo. Mchezaji Max Nzengeli wa Young Africans alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Max Nzemgeli akiwa na tuzo yake

AZAM YATAKATA KMC COMPLEX.

TIMU ya Azam imeendeleza ubabe wake dhidi ya timu ya KMC baada ya kuifunga 0-2 katika mchezo uliopigwa leo kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo timu zote zilikuwa zikiutaka mchezo na zilishambuliana kwa kasi licha ya Azam kuutawala mchezo huo lakini hadi dakika 45 zinatamatika hakuna aliyefanikiwa kuguza nyavu za mwenzake kwa bao.

Akaminko (kushoto) akipambana namchezaji wa KMC

Kipindi cha pili dakika ya 55 ya mchezo mchezaji wa Azam Iddy Seleiman alifungua ukurasa wa mabao wa timu hiyo na kurejea tena kambani dakika ya 64 ya mchezo huo na kufanya Azam kuongoza kwa mabao mawili.

Hadi mwamuzi wa mchezo huo Ramadhani Kayoko anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalisalia 0-2 na kuifanya KMC kuendelea kuburuza ‘mkia’ wa Ligi Kuu ya NBC huku Iddy Selemani akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

SINGIDA YAONGEZA MAUMIVU KWA MTIBWA.

SINGIDA Black Stars imejipata baada ya kuifunga timu ya Mtibwa Sugar mabao 3-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa leo katika uwanja wa Jamhuri Dodoma majira ya saa nane mchana.

Iliwachukua dakika tano pekee Singida kufungua ukurasa wa mabao kupitia mchezaji wao Nduhumwe Mosi na dakika ya 16 Horso Muaku aliiongezea timu hiyo bao la pili hivyo kwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao mawili.

Wachezaji wa Singida wakishangilia bao.

Kipindi ca pili timu zote zilikuwa na ari ya kutaka ushindi hasa Mtibwa iliyokuwa nyuma kwa mabao mawili hata hivyo ndoto zao zilizidi kudidimia baada ya Kennedy Juma kuongeza bao la tatu kwa timu ya Singida ikiwa ni dakika ya 58 ya mchezo huo.

Dakika ya 88 Mtibwa ilipata bao la kufutia machozi kupitia mchezaji wao Raizin Haji hivyo kufanya mchezo kumalizika wa 1-3 na Singida kufanikiwa kubeba alama zote tatu ugenini huku mchezaji wa Singida Horso Muaku alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

DODOMA JIJI WAJIPATA JAMHURI

Timu ya Dodoma Jiji imejipata katika uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri baada ya kuhakikisha wanashinda kila mchezo wawapo hapo.

Dodoma ambayo imecheza na timu ya TRA United jana imefanikiwa kushinda michezo minne katika uwanja huo,sare mbili na huku ikipoteza mchezo mmoja tu katika michezo saba ambayo timu hiyo imecheza uwanjani hapo.

Mchezaji wa Dodoma Jiji,Dickson Mhilu

Katika mchezo wa jana ulionza majira ya saa moja usiku Dodoma ilionekana ikizitaka alama zote tatu kutoka kwa TRA kwani timu hiyo ilitawala mchezo ambapo dakika ya 15 ya mchezo huo Faraji Kayanda alifungua ukurasa wa mabao.

TRA nayo ilionekana ikiuta ka mchezo kwa kutaka kusawazisha hata hivyo ndoto yao ilizimwa na mchezaji wa Gadiel Michael ambaye aliongeza bao la pili kwa timu yake hivto kwenda mapumziko Dodoma ikiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilirejea ambapo dakika ya 55 Edgar William alizidi kudidimiza matumaini ya TRA baada ya kuongeza bao la tatu kwa timu yake ambapo mpaka mchezo unatamatika Dodoma iliibuka na ushindi wa 3-0 hivyo timu hiyo ilipanda kutoka nafasi ya saba hadi ya sdita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
[13/02/2026, 09:26:53] Honest Tplb: mkuu

LIGI KUU YA NBC ‘KUCHANJA MBUGA’ LEO.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili itakayochezwa katika mikoa ya Mwanza kwenye uwanja wa CCM Kirumba na Mbeya kwenye uwanja wa Sokoine.

Mchezo wa kwanza utakuwa saa 8:00 mchana ambapo timu ya Pamba Jiji ya Mwanza itaialika timu ya Coastal Union ya Tanga katika ‘dimba’ la Kirumba.

Pamba Jiji inashika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 12 ikishinda minne, sare tano na kufungwa mitatu huku ikikusanya alama 17.

Coastal ipo nafasi ya 12 katika msimamo ikicheza michezo 12 ikishinda miwili, sare tano na kufungwa michezo mitano huku ikikusanya alama 11.

Mchezo wa pili leo utakuwa majira ya saa 10:15 alasiri ambapo timu ya Tanzania Prisons itaialika timu ya Mashujaa katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.

Prisons ipo nafasi ya 15 ikiwa imekusanya jumla ya alama nane ikiwa imeshinda michezo miwili, sare mbili na kufungwa michezo sita.