Category: STORY

MICHEZO MIWILI KUHITIMISHA MZUNGUKO WA 27 NBC CHAMPIONSHIP LEO.

 

MZUNGUKO wa 27 Ligi ya NBC Championship unahitimishwa leo kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Shinyanga na Morogoro.

Mkoani Shinyanga Stand United itaialika Green Warriors kwenye uwanja wa CCM Kambarage saa 8:00 mchana.

Stand United na Green Warriors zinapambana kutoka katika mstari wa kucheza mtoano wa kushuka daraja hivyo kufanya mchezo wa leo kuwa wa muhimu kwa pamde zote mbili.

Stand United ipo nafasi ya 11 na alama 30 kwenye michezo 26 iliyocheza huku Green Warriors ikiwa nafasi ya 12 na alama 27 kwenye michezo 26.

Mkoani Morogoro Transit Camp itaialika Biashara United kwenye uwanja wa Jamhuri saa 10:00 alasiri.

Transit Camp ipo nafasi mbaya kwenye msimamo ikiwa nafasi ya 13 na alama zake 23 kwenye michezo 26 huku Biashara ikihitaji ushindi ili kuzidi kuweka hai mbio za kuwania kupanda Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 ikiwa na alama 53 kwenye michezo 26 mpaka sasa.

KEN GOLD KINARA WA USHINDI NBC CHAMPIONSHIP.

 

MICHEZO 208 imechezwa ndani ya Ligi ya NBC Championship sawa na michezo 26 kwa kila timu huku jumla ya mabao 490 yakifungwa mpaka sasa.

Ken Gold kinara wa Ligi ya NBC Championship ndio timu iliyoshinda michezo mingi mpaka sasa ikishinda 18 huku ikifunga mabao 44 na kufungwa 15.

Pamba, Biashara na Mbeya Kwanza zinafuatia kila mmoja ikishinda michezo 16 Kati ya 26 iliyocheza mpaka sasa.

Pamba inashika nafasi ya pili ikiwa na alama 55 huku Biashara United na Mbeya Kwanza zikifuatia kila mmoja ikiwa na alama 53 zikitofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa Biashara ikiwa na tofauti ya mabao 29 huku Mbeya Kwanza ikiwa na 17.

Ruvu Shooting ndio timu iliyoshinda michezo michache zaidi ikifanya hivyo mara mbili pekee kwenye michezo 26 iliyocheza mpaka sasa huku ikishika nafasi ya mwisho kwenye Ligi ya NBC Championship.

MBEYA KWANZA YAIBAMIZA BIASHARA NBC CHAMPIONSHIP IKIENDELEA.

 

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Machi 24, 2024 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Mtwara na Morogoro.

Mkoani Mtwara saa 10:00 alasiri Mbeya Kwanza ikaibamiza Biashara United kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, bao pekee la Mbeya Kwanza likifungwa na Magata Charles Dakika ya 90+4 ya mchezo.

Kwa Matokeo haya Mbeya Kwanza inapanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo ikifikisha alama 53 sawa na Biashara United ikizidiwa utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa Biashara ikiwa na 29 huku Mbeya Kwanza ikiwa na 17.

Mchezo mwengine ukazikutanisha Transit Camp dhidi ya Cosmopolitan saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kumalizika kwa Transit Camp kufungwa 1-2 mbele ya Cosmopolitan.

Mzunguko wa 26 utamatika kesho kwa mchezo Kati ya Green Warriors dhidi ya Pan Africans kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani sa 10:00 alasiri.

KENGOLD, PAMBA HAKUNA MBABE NBC CHAMPIONSHIP.

MICHEZO mitatu ya Ligi ya NBC Championship imechezwa leo kwenye viwanja mbalimbali ndani ya mikoa mitatu tofauti.

Mchezo wa mapema zaidi leo ulichezwa mkoani Arusha Kati ya Polisi Tanzania na Mbuni kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid na kumalizika kwa Polisi kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Mchezo uliosubiriwa kwa hamu zaidi leo Ken Gold dhidi ya Pamba uliopigwa kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya umemalizika kwa sare ya mabao 2-2 hivyo kila timu kugawana alama na kubaki kwenye nafasi zao.

Mchezo mwengine wa saa 10:00 alasiri Kati ya Copco na Mbeya City kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza umemalizika kwa sare ya mabao 2-2.

KENGOLD, PAMBA HAPATOSHI NBC CHAMPIONSHIP LEO.

 

MZUNGUKO wa 26 wa Ligi ya Championship ya NBC unaendelea tena leo kwa michezo mitatu na itakayorushwa mubashara kupitia chaneli za TV3 na ST BONGO ndani ya king’amuzi cha StarTimes.

Mapema saa 8:00 mchana Polisi Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mbuni kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Mchezo unaosubiriwa kwa hamu leo ni kati ya Ken Gold na Pamba utakaopigwa saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.

Mchezo huu unatazamwa sana kutokana na nafasi ya kila timu kwenye msimamo Ken Gold ikiwa nafasi ya kwanza na Pamba ikiwa nafasi ya pili huku timu hizo zikipishana kwa alama tano.

Ken Gold inahitaji ushindi kwenye mchezo Huu ili kuzidi kujikita kileleni na kuendelea kushikilia rekodi yake ya kutopoteza mchezo wowote nyumbani huku Pamba ikihitaji ushindi ili kupunguza utofauti wa alama uliopo.

Mchezo wa mwisho leo utapigwa saa 10:00 alasiri ukizikutanisha Copco dhidi ya Mbeya City kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.