Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

LIGI KUU YA NBC

LIGI KUU YA NBC KUCHEZWA ARUSHA, SINGIDA LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Februari 7, 2025 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Arusha na Singida kuanzia saa 10:00 Alasiri.

Mkoani Arusha Coastal Union itaikaribisha JKT Tanzania kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid huku ikiingia kwenye mchezo huu ikishika nafasi ya 11 ikikusanya alama 18 kwenye michezo 16 na JKT Tanzania ikishika nafasi ya nane baada ya kukusanya alama 19 wakiwa na tofauti ya alama moja (1) pekee kati yao.

Mkoani Singida, timu ya Singida Black Stars itakuwa mwenyeji wa Kagera Sugar ya mkoani Kagera kwenye uwanja wa CCM Liti huku mara ya mwisho timu hizi kukutana Agosti 24, 2024 mkoani Kagera, Singida Black Stars iliibuka na ushindi wa bao 1-0 likifungwa na Mchezaji Anthony Tra Bi dakika ya 90+3 ya mchezo huo.

Michezo hii miwili inakamilisha michezo ya mzunguko wa 17 wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 ambapo mpaka sasa timu ya Young Africans ikishika usukani na alama 45 huku Kengold ikiburuza mkia ikiwa na alama sita pekee.

 

FOUNTAIN GATE,SIMBA WATOSHANA NGUVU LIGI KUU NBC.

LIGI Kuu ya NBC imeendelea jana  mkoani Manyara ambapo  timu ya Fountain Gate Iliwakaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa majira ya saa kumi alasiri.

Mchezo huo ulianza kwa kasi ambapo timu zote zilionekana kushambuliana kwa kasi kubwa  huku kila timu ikionyesha nia ya kuzitaka  alama tatu muhimu za mchezo huo jambo lilipolekea kwenda mapumziko wakiwa hawajafungana .

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya  57 mshambuliaji wa Simba, Leonel Ateba alifunga bao la  kwanza kwa timu yake   hivyo Simba kuwa mbele kwa  0-1.

Dakika ya 74 winga wa Simba Ladack Chasambi alijifunga goli  baada ya kupiga mpira  nyuma na golikipa wa Simba Moussa Camara  kushindwa kuumudu  ukaingia  nyavuni hivyo ubao kusomeka 1-1 mpaka mchezo huo unatamatika.

Simba ilifanikiwa kuvuna alama moja ugenini na kufikisha alama 44  wakiwa nafasi ya pili ya msimamo wakiwa wamefunga mabao 35 na kufungwa 6 katika mechi 17 ilizocheza mpaka sasa.

 

LIGI KUU YA NBC

LIGI KUU YA NBC KUCHEZWA VIWANJA VINNE LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea kwa mzunguko wa 17 huku mechi nne zikichezwa katika viwanja mbalimbali nchini kuanzia majira ya saa nane mchana.

Mchezo wa kwanza utachezwa saa nane mchana katika  uwanja wa Jamhuri Dodoma ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza .

Sambamba na mchezo huo Tanzania Prisons “wajelajela” watawakaribisha timu ya Mashujaa “Wana mapigo na mwendo” katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya  muda ikiwa ni saa nane mchana.

Mchezo  wa tatu  kwa siku ya leo ni timu ya Fountain Gate watawakaribisha  timu ya Simba katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo Babati Mkoani Manyara saa kumi alasiri.

Mkoani Dar es Salaam wenyeji wa  uwanja wa Chamazi  timu ya Azam watawakaribisha timu ya KMC “Kinoboys” katika mchezo utakaochezwa saa moja jioni.

 

MZIZE,DUBE HAWASHIKIKI LIGI KUU NBC

WASHAMBULIAJI wa Yanga Prince Dube na Clement Mzize wameongeza kasi katika mbio za ufungaji bora baada ya kufung mabao mawili kila mmoja katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya KenGold mchezo uliochezwa leo katika uwanja wa KMC.

Licha ya Kocha Mkuu wa Yanga Saed Ramovic kuaga jana ikiwa ni saa chache kuelekea mechi yao dhidi ya KenGold Yanga imefanikiwa kufunga mabao 6-1 .

Prince Dube ndio alifungua ukurasa wa mabao ikiwa ni dakika ya pili ya mchezo huo kabla ya Mzize  kufunga baola pili dakika ya sita ya mchezo huo huku Pacome Zouzuoa akiongeza bao la tatu dakika ya 39 dakika  nne mbele Mzize alirudi tena na kufunga bao la nne huku Dube akiongeza bao la tano dakika ya 43 y mchezo huo na kuwafanya Yanga kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 5-0.

Kipindi cha pili kilianza huku Yanga wakionekana kuzidi kulisakama lango la kenGold  licha ya timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji  ambapo Yanga dakika ya 85 Duke Abuya aliongeza bao la 6 kwa  timu yake.

KenGold walipata bao la kujifutia machozi kupitia mchezaji wake Seleman Rashid baada ya kupiga mpira mrefu ambao ulimshinda kipa wa Yanga Djigui Diarra hivyo mchezo kutamatika kwa 6-1.

Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mchezo huo.

Ligi Kuu itaendelea kesho kwa michezo minne ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba,Tanzania Prisons dhidi ya Mashujaa,Fountain Gate wakiwakaribisha Simba na Azam watacheza na KMC .

CHIKOLA AWALIZA NAMUNGO LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo mkoani Tabora kwa mchezo uliozikutanisha  timu ya Tabora United dhidi ya  timu ya Namungo  katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Mchezo huo uliochezwa majira ya saa nane mchana  ulianza kwa kasi tangu mwanzo kwani dakika ya nne ya mchezo huo mchezaji wa Namungo, Jacob Massawe aliweka mpira wavuni mwa Tabora United.

Offen Chikola ndio alirejesha matumaini ya Tabora United katika dakika ya 32 ya mchezo huo ambapo alifunga bao na hivyo kuifanya mechi kwenda mapumziko wakiwa sare ya 1-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo dakika ya 52 mshambuliaji wa Tabora Heritier Makambo aliiongezea bao la pili timu yake na kufanya ubao kusomeka 2-1 pasi ya mwisho ikiwa imetolewa na Offen Chikola.

Mchezo ulitamatika kwa timu ya Tabora kubeba alama zote tatu mhimu za mchezo huo na mchezaji wao Offen Chikola akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.