Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

SIMBA WAENDELEZA UBABE DHIDI YA TABORA UNITED

Ligi Kuu ya NBC  ambayo ni Ligi ya nne kwa ubora barani Afrika imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United waliwakaribisha Simba katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Mchezo huo umeanza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kucheza kwa tahadhari kwani mchezo huo ulitawaliwa na tambo za Tabora kuwafunga Azam uwanja wa Ali Hassan Mwinyi  na Yanga katika uwanja wa Azam Complex.

Dakika 12 ziliwatosha Simba kufungua akaunti ya mabao kupitia  mshambuliaji wao Leonel Ateba kisha dakika ya 34 kuongeza bao la pili kupitia mkwaju wa penati hivyo kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili .

Kipindi cha pili Simba walizidi kulisakama lango laTabora  licha ya timu hiyo kufanya mabadiliko kwa  wachezaji wawili  lakini Simba walikuwa wakicheza kwa kasi na ufundi mwingi dakika ya 67 beki wa Simba Shomari Kapombe aliongeza bao kwa timu yake akipokea pasi kutoka kwa Leonel Ateba  akififisha matumaini ya Tabora United kurejesha mabao hao.

Dakika 90 za mchezo huo zimetamatika kwa Simba kuendekeza ubabe  kwani tangu Tabora United wapande daraja hawajawahi kuwafungana leo wakiondoka na mabao matatu huku mchezaji  Leonel Ateba akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Simba wamerejea kileleni wakiwa wamefikisha alama 43 wakifunga mabao 34 huku wakiruhusu mabao matano katika michezo 16 ya Ligi Kuu ya NBC waliyocheza .

LADHA ZA LIGI KUU NBC ZAREJEA YANGA WAKIWALIZA KAGERA SUGAR

Ladha za Ligi Kuu ya NBC zimerejea rasmi leo Februari 1 kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam ambapo timu ya Yanga waliwakaribisha Kagera Sugar.

Mchezo ulianza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kushambuliana kwa kasi huku Yanga wakionekana kuutawala mchezo.

Ilimchukua dakika 32 mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize kufungua akaunti ya mabao na kuifanya timu yake kwenda kifua mbele mapumziko licha ya kiungo wa timu hiyo Aziz Ki kushindwa kufunga mkwaju wa penati waliopata timu yake.

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya 60 Mudathir Yahya aliongeza bao la pili kwa Yanga huku wakionekana kuzidi kulisaka lango la mpinzani wao na kutaka mabao zaidi.

Pacome Zouzoua aliongeza bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Kagera Sugar kumfanyia madhambi Max Nzengeli  kabla ya Kennedy Musonda kufunga bao la nne hivyo Yanga kufikisha alama 42 wakiwa wamefunga mabao 36 na wakiruhusu 6.Mchezaji wa Yanga Max Nzegeli amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Ladha za Ligi Kuu ya  NBC zitaendelea kesho mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United watawakaribisha Simba saa kumi alasiri katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

LIGI KUU NBC KUREJEA WIKIENDI .

Ligi Kuu ya NBC ligi ya nne kwa ubora barani Afrika inarejea wikiendi hii febuari 1 baada ya mapumziko ya takribani mwezi mmoja .

Ligi hiyo itaanza kwa michezo miwili ya viporo vya mzunguko wa 16 ambavyo ni mechi za Yanga dhidi ya Kagera Sugar Februari 1 katika uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam.

Februari 2 Tabora United itakuwa mwenyeji wa Simba katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora katika mchezo uliokuwa umepangiwa tarehe mpya.

Mzunguko wa 17 utaanza rasmi februari tano hadi saba kwa michezo nane itakayochezwa katika viwanja mbalimbali nchini .

Akizungumza kuhusu kurejea kwa Ligi Afisa Habari wa Bodi ya Ligi (TPLB), Karim Boimanda amesema kuwa maandalizi yote yako tayari na kwa upande wa usimamizi Bodi iko tayari, timu, viwanja vimekaguliwa ubora wake viko na upande wa ratiba ilishatoka mapema” Amesema Boimanda na kuongeza kuwa

“Mapumziko ya Ligi yalitokana na uwepo wa michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyochezwa mwanzoni mwa mwezi januari kisiwani Pemba na pia uwepo wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani yaani CHAN ambazo zilipaswa kufanyika februari kabla ya kusogezwa mbele hadi agosti 2 ambapo Tanzania,Kenya na Uganda ni nchi zinazoandaa michuano hiyo”.

LIGI KUU NBC YA NNE KWA UBORA AFRIKA

Shirikisho la Kimataifa la Historia na Takwimu za Mpira wa Miguu (IFFHS) limeitangaza Ligi Kuu ya Tanzania (NBC Premier League) kuwa Ligi ya nne kwa ubora barani Afrika na ya 57 duniani kwa mwaka 2024.

Ligi hiyo imepanda kwa nafasi mbili kutoka nafasi ya sita mwaka 2023 hadi nafasi ya nne ikizipiku Ligi za Afrika Kusini na Tunisia.

Kwa mujibu wa taarifa ya IFFHS kwa upande wa Afrika nchi zilizoko chini ya Shirikisho la Soka (CAF) Ligi Kuu ya Misri inayofahamika kama Nile Premier League ndio kinara kwa ubora Afrika.

Nafasi ya pili inashikiliwa na Botola Pro ambayo ni Ligi Kuu ya Morocco huku League 1 ya Algeria ikishika nafasi ya tatu kwa ubora mwaka 2024.

Kwa upande wa Ligi Kuu ya NBC ya Tanzania imekwea hadi nafasi ya nne barani Afrika kutokana na ligi hiyo kuwa na usimamizi bora kuanzia Serikali, Shirikisho la Soka nchini (TFF), Bodi ya Ligi Kuu (TPLB), Klabu zinazoshiriki ligi hiyo, wadhamini mbalimbali wanavyounga mkono pamoja na mashabiki.

HAWA HAPA WASHINDI WA TUZO ZA NBC DESEMBA.

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Clement Mzize amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu ya NBC huku Kocha wa Yanga Sead Ramovic akichaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi huo.

Mzize amewashinda Prince Dube wa Yanga na Feisal Salum wa Azam alioingia nao fainali za tuzo hizo baada ya kufunga mabao 4 na kutoa pasi za mwisho 3 katika dakika 288 alizocheza ndani ya mwezi huo.

Yanga ilizifunga Tanzania Prisons mabao 4-0, Dodoma Jiji 0-4 Mashujaa 3-2, na Fountain Gate mabao 5-0 hivyo kukusanya alama 12.

Aidha Kocha wa Yanga Sead Ramovic amefanikiwa kuwa kocha Bora wa mwezi huo baada ya kuwashinda Davis Fadlu wa Simba na Rachid Taoussi wa Azam baada ya kuiongoza Yanga kushinda michezo minne ambayo timu yake ilicheza ndani ya mwezi huo na kupanda kutoka nafasi ya tatu hadi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Kamati ya Tuzo pia imemchagua Meneja wa uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Dar es Salaam, Ashraf Omar kuwa Meneja bora wa uwanja mwezi desemba kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo na masuala ya miundombinu.

Kwa upande wa Ligi ya Championship ya NBC kamati imemchagua mchezaji wa Mbeya City, Kilaza Mazoea kuwa mchezaji bora wa Ligi hiyo kwa mwezi desemba baada ya kufunga mabao manne katika dakika 234 alizocheza akiwashinda Elias Maguri wa Geita Gold/Biashara na Emmanuel Maziku wa Stand United.

Kocha wa Mbeya City Salum Mayanga, amechaguliwa kuwa kocha bora wa ligi hiyo kwa mwezi desemba ambapo aliiongoza timu yake kushinda michezo 3 na kufanikiwa kupanda kutoka nafasi ya sita hadi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo akiwashinda Awadh Juma wa Mtibwa na Maka Mwalwisi wa TMA alioingia nao fainali.

Mbeya City walizifunga timu za Polisi Tanzania 4-0,Geita Gold 1-0 na Cosmopolitan 1-0.