TAYARI mizunguko 19 ya Ligi ya Championship ya NBC imeshachezwa hadi sasa na kushuhudiwa kwa ushindani mkubwa wa nafasi kwenye msimamo wa ligi hiyo.
Mtibwa Sugar inaendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ikiwa na alama 45 ikifuatiwa na Geita Gold kwenye nafasi ya pili ikiwa na alama 42, Stand United ipo nafasi ya tatu ikiwa na alama 39 huku nafasi ya nne ikishikiliwa na Mbeya City ikiwa na alama 39.
Biashara United inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama nne pekee hadi sasa, Cosmopolitan inashikilia nafasi ya 15 moja kutoka mwisho ikiwa na alama tisa.
Timu mbili za juu kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC zinapanda moja kwa moja Ligi Kuu ya NBC huku zile mbili za mwisho zikishuka moja kwa moja hadi First League.
 
					 
		 
		 
		