Tag: #NBCCL#STORY

COASTAL, JKT KUANZA NYUMBANI LEO LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI Kuu ya NBC inarejea leo Septemba 29 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Tanga na Shinyanga.

JKT Tanzania watakuwa wenyeji wa Kagera Sugar katika uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga saa 10 alasiri huku ukiwa mchezo wa kwanza wa JKT Tanzania kucheza nyumbani tangu kupanda Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2023/2024.

Coastal Union itacheza kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga saa 1:00 usiku dhidi ya Tabora United huku Coastal ikiwa haijapata ushindi wowote msimu huu.

TMA, KEN GOLD, COPCO ZAPETA NBC CHAMPIONSHIP

TIMU za TMA ya Arusha, Ken Gold ya Mbeya na Copco FC ya Mwanza zimefanikiwa kushinda michezo yao kwenye Ligi ya NBC Championship kwa mara ya kwanza msimu huu.

TMA ilicheza mapema saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kushinda 1-0 dhidi ya Biashara ya Mara.

Ushindi huo umeifanya TMA kufikisha alama nne na kukaa nafasi ya nne ikiwa haijafungwa mchezo wowote mpaka sasa huku ikiwa mojawapo ya timu tatu zilizopanda daraja kutoka First League.

Ken Gold imeifunga Green Warriors ya Dar kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya na kufikisha alama nne zinazowaweka nafasi ya tatu huku wakiwa hawajapoteza mchezo mpaka mzunguko wa pili.

Kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Copco imepata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Cosmopolitan ya Dar I’m na kusogea mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi ya NBC Championship.

Cosmopolitan imeshindwa kupata alama yoyote mpaka mzunguko wa pili ikipoteza michezo yote miwili na kuruhusu jumla ya mabao saba.

Ligi ya NBC Championship itaendelea tena kesho Septemba 17, kwa michezo mitatu huku kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mbuni itacheza na Stand United saa 8:00 mchana, FGA Talents dhidi ya Mbeya Kwanza kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Mbeya City dhidi ya Transit Camp kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya huku michezo hiyo miwili ikianza saa 10:00 alasiri .

PAMBA YAANZA KIBABE NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Septemba 11 kwa mchezo mmoja kuchezwa kati ya Pamba Jiji ya Mwanza na Cosmopoilitan ya Dar uliomalizika kwa Cosmo kupoteza kwa mabao 4-0.

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza umeshuhudiwa Cosmo waliokuwa mabingwa wa First League msimu wa 2022-2023 wakienda mapumziko wakiwa wameruhusu mabao matatu.

“Hii timu ina malengo yake, niliwaambia wachezaji tunahitaji sana kupanda Ligi Kuu ya NBC na endapo tukifungwa sana isiwe zaidi ya mechi mbili na wametekeleza majukumu tumeweza kupata ushindi” amesema kocha mkuu wa Pamba Mbwana Makata.

Kwa ushindi huo Pamba imepanda moja kwa moja kileleni mwa msimamo wa Ligi ya NBC Championship kwa tofauti ya idadi ya mabao juu ya timu za Mbeya City, Pan Africans na FGA Talents walioshinda michezo yao kwanza kama ilivyo kwa Pamba.

NBC CHAMPIONSHIP YAPAMBA MOTO

LIGI ya NBC Championship imeendelea Leo Septemba 10 kwa michezo minne kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Mchezo wa mapema saa 8:00 mchana ulizikutanisha TMA na Stand United katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kumalizika kwa suluhu.

Mchezo mwengine ulizikutanisha Mbuni na Biashara United saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kumalizika kwa sare ya bao moja.

KenGold wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani Sokoine mkoani mbeya wakagawana alama na Transit Camp kwa sare ya bao moja.

FGA Talents imekuwa timu pekee kwa siku ya leo kuondoka na alama tatu baada ya kuwafunga Ruvu shooting mabao 2-1 kwenye uwanja wa Jamnhuri mkoani Morogoro.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho Septemba 11 kwa mchezo mmoja kuchezwa Pamba wakiwaalika Cosmopolitan kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.

NBC CHAMPIONSHIP KUENDELEA TENA LEO.

PAZIA la Ligi ya NBC Championship lilifunguliwa rasmi jana septemba, 9 kwa michezo mitatu kuchezwa.

Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa michezo minne kati ya TMA na Stand United kwenye uwanja Sheikh Amri Abeid,Arusha saa 8:00 mchana.

Mchezo wa pili utazikutanisha Ken Gold dhidi ya Transit Camp uwanja wa Sokoine, Mbeya saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa tatu ni Kati ya FGA Talents na Ruvu Shooting uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro saa 10:00 alasiri na Mchezo wa mwisho Mbuni atakuwa mwenyeji wa Biashara United kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha saa 10:00 alasiri.