GOLIKIPA wa timu ya Simba Moussa Camara ameendeleza ubabe wake kwa kuendelea kukaa kileleni kwa kuwa na hati safi (Cleansheet) nyingi (17) kuliko magolikipa wenzake wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu 2024/2025.
Camara ambaye ni msimu wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu ya NBC amefanikiwa kukusanya hati safi hizo katika michezo 25 ya Ligi Kuu aliyocheza mpaka sasa huku akifanikiwa kuendelea kuwa juu ya msimamo wa hati safi huku Djigui Diarra wa Young Africans akiwa nafasi ya pili baada ya kukusanya hati safi 15.
Patrick Munthali wa Mashujaa anashikilia nafasi ya tatu akiwa na hati safi 12 huku Mohamed Mustapha wa Azam na Yona Amos wa Pamba Jiji wakiwa nazo 10 kila mmoja.
Yakoub Suleiman wa JKT Tanzania nae hayuko mbali akiwa amefanikiwa kukusanya hati safi 8 huku Metacha Mnata wa Singida Black Stars na Ngaleka Katembua wa Dodoma Jiji wakiwa wamefanikiwa kukusanya hati safi 7 kila mmoja huku ikisalia mizunguko miwili kutamatika kwa msimu wa 2024/25.


