Category: STORY

CAMARA ‘ANG’ANG’ANIA’ KILELENI HATI SAFI LIGI KUU YA NBC.

GOLIKIPA wa timu ya Simba Moussa Camara ameendeleza ubabe wake kwa kuendelea kukaa kileleni kwa kuwa na hati safi (Cleansheet) nyingi (17) kuliko magolikipa wenzake wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu 2024/2025.

Camara ambaye ni msimu wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu ya NBC amefanikiwa kukusanya hati safi hizo katika michezo 25 ya Ligi Kuu aliyocheza mpaka sasa huku akifanikiwa kuendelea kuwa juu ya msimamo wa hati safi huku Djigui Diarra wa Young Africans akiwa nafasi ya pili baada ya kukusanya hati safi 15.

Patrick Munthali wa Mashujaa anashikilia nafasi ya tatu akiwa na hati safi 12 huku Mohamed Mustapha wa Azam na Yona Amos wa Pamba Jiji wakiwa nazo 10 kila mmoja.

Yakoub Suleiman wa JKT Tanzania nae hayuko mbali akiwa amefanikiwa kukusanya hati safi 8 huku Metacha Mnata wa Singida Black Stars na Ngaleka Katembua wa Dodoma Jiji wakiwa wamefanikiwa kukusanya hati safi 7 kila mmoja huku ikisalia mizunguko miwili kutamatika kwa msimu wa 2024/25.

HATMA YA GEITA, STAND KUJULIKANA LEO .

HATMA ya kucheza mchezo wa mtoano kushiriki Ligi Kuu ya NBC kujulikana leo ambapo timu ya Stand United itakuwa mwenyeji wa Geita Gold kwenye uwanja wa CCM kambarage, Shinyanga saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Nyankumbu ulimalizika kwa Sare ya mabao 2-2 hivyo kuufanya mchezo wa leo kuwa mgumu zaidi timu zote zikitafuta nafasi ya kucheza Ligi Kuu ya NBC.

Ushindi, suluhu au sare ya bao 1-1 unaipa nafasi Stand United kusonga mbele kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa Faida ya mabao ya ugenini.

Ushindi au sare ya mabao 3-3 na kuendelea unaipa Geita Gold nafasi ya kuendelea kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa faida ya mabao mengi ya ugenini.

Mshindi wa jumla wa michezo hii ya mtoano wa kupanda (Promotions Playoffs) atacheza na timu iliyofungwa kwenye mchezo wa mtoano utakaozikutaisha timu iliyoshika nafasi ya 13 na 14 kwenye Ligi Kuu ya NBC.

SIMBA, SINGIDA BS KINAPIGWA LIGI KUU NBC LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Mei 28 kwa mchezo mmoja wa kukamilisha mzunguko wa 28 Kati ya Simba na Singida Black Stars katika uwanja wa KMC, Dar es Salaam.

Katika mchezo wa mwisho timu hizo kukutana mkoani Singida timu ya Singida ilikubali kichapo cha bao 0-1 mbele ya Simba kwenye uwanja wake wa Nyumbani CCM Liti bao likifungwa na Fabrice Ngoma.

Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 69 ikishinda michezo 22 ikitoka sare michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja pekee.

Singida Black Stars ipo nafasi ya 4 kwenye msimamo ikiwa na alama 53 baada ya kushinda michezo 16 ikitoka sare mitano na kupoteza michezo sita.

KILUVYA

KILUVYA YASALIA LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC.

TIMU ya Kiluvya ya Mkoani Pwani imefanikiwa kubakia kwenye Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu unaofuata baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Transit Camp hivyo kufanikiwa kubaki kwa ushindi wa jumla (aggregate) wa mabao 4-3.

 

 

Mchezo wa kwanza uliochezwa wiki iliyopita kwenye uwanja wa TFF Technical Center – Kigamboni Transit Camp iliibuka na ushindi wa mabao 3-2.

 

Kiluvya iliyopanda daraja kutoka ligi ya First League haikuwa na msimu bora baada ya kumaliza ligi ikiwa imefunga mabao machache (19) sawa na timu ya Cosmopolitan iliyoshuka daraja.

Transit Camp sasa itacheza na Rhino Rangers ya mkoani Tabora kuwania kubakia kwenye Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu ujao wa 2025/2026.

 

Rhino imepata nafasi ya kucheza mchezo huo baada ya kuitoa timu ya Nyumbu kwa tofauti ya mabao 5-3 na itafanikiwa kupanda ligi ya Championship ya NBC ikiwa itaifunga timu ya Transit Camp kwa tofauti kubwa ya mabao kwenye mchezo wa nyumbani na ugenini.

FIRST LEAGUE KUHITIMISHWA LEO.

KMC YAFUFUA MATUMAINI YA KUSALIA LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja kati ya Tabora United iliyokuwa mwenyeji wa KMC kwenye dimba la Alli Hassan Mwinyi mkoani Tabora saa 10:00 na kumalizika Tabora United kupoteza kwa bao moja.

Deogratius Anthony wa KMC ndiye aliyeibuka shujaa wa KMC kwani bao lake la dakika ya 59 ndio lilipeleka maumivu kwa Tabora na kuifanya KMC kufikisha alama 33 na kupanda kutoka nafasi ya 13 hadi ya 9 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC huku ikisalia michezo miwili kumalizika kwa msimu.

Tabora United imeendeleza rekodi mbaya baada ya kupoteza mchezo wa sita mfululizo kwenye Ligi Kuu ya NBC ikisalia nafasi ya tano na alama 37 mbili zaidi ya JKT inayoshika nafasi ya sita.

Mchezaji wa KMC Deogratius Anthony alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kufunga bao pekee lililoleta utofauti kwenye mchezo huo.