Category: STORY

SIMBA WAENDELEZA UBABE DHIDI YA TABORA UNITED

Ligi Kuu ya NBC  ambayo ni Ligi ya nne kwa ubora barani Afrika imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United waliwakaribisha Simba katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Mchezo huo umeanza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kucheza kwa tahadhari kwani mchezo huo ulitawaliwa na tambo za Tabora kuwafunga Azam uwanja wa Ali Hassan Mwinyi  na Yanga katika uwanja wa Azam Complex.

Dakika 12 ziliwatosha Simba kufungua akaunti ya mabao kupitia  mshambuliaji wao Leonel Ateba kisha dakika ya 34 kuongeza bao la pili kupitia mkwaju wa penati hivyo kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili .

Kipindi cha pili Simba walizidi kulisakama lango laTabora  licha ya timu hiyo kufanya mabadiliko kwa  wachezaji wawili  lakini Simba walikuwa wakicheza kwa kasi na ufundi mwingi dakika ya 67 beki wa Simba Shomari Kapombe aliongeza bao kwa timu yake akipokea pasi kutoka kwa Leonel Ateba  akififisha matumaini ya Tabora United kurejesha mabao hao.

Dakika 90 za mchezo huo zimetamatika kwa Simba kuendekeza ubabe  kwani tangu Tabora United wapande daraja hawajawahi kuwafungana leo wakiondoka na mabao matatu huku mchezaji  Leonel Ateba akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Simba wamerejea kileleni wakiwa wamefikisha alama 43 wakifunga mabao 34 huku wakiruhusu mabao matano katika michezo 16 ya Ligi Kuu ya NBC waliyocheza .

LADHA ZA LIGI KUU NBC ZAREJEA YANGA WAKIWALIZA KAGERA SUGAR

Ladha za Ligi Kuu ya NBC zimerejea rasmi leo Februari 1 kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam ambapo timu ya Yanga waliwakaribisha Kagera Sugar.

Mchezo ulianza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kushambuliana kwa kasi huku Yanga wakionekana kuutawala mchezo.

Ilimchukua dakika 32 mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize kufungua akaunti ya mabao na kuifanya timu yake kwenda kifua mbele mapumziko licha ya kiungo wa timu hiyo Aziz Ki kushindwa kufunga mkwaju wa penati waliopata timu yake.

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya 60 Mudathir Yahya aliongeza bao la pili kwa Yanga huku wakionekana kuzidi kulisaka lango la mpinzani wao na kutaka mabao zaidi.

Pacome Zouzoua aliongeza bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Kagera Sugar kumfanyia madhambi Max Nzengeli  kabla ya Kennedy Musonda kufunga bao la nne hivyo Yanga kufikisha alama 42 wakiwa wamefunga mabao 36 na wakiruhusu 6.Mchezaji wa Yanga Max Nzegeli amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Ladha za Ligi Kuu ya  NBC zitaendelea kesho mkoani Tabora ambapo timu ya Tabora United watawakaribisha Simba saa kumi alasiri katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

HAWA HAPA WAKALI WA NAMBA LIGI KUU YA NBC.

Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kurejea tena Februari 1, 2025 kwa mchezo mmoja kati ya Young Africans na Kagera Sugar saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa KMC Complex.

Mpaka Ligi inasimama Desemba 29, 2024 jumla ya mabao 266 yalifungwa huku Mchezaji Elvis Rupia wa Singida Black Stars akiongoza kwa ufungaji akiwa na mabao nane akifuatiwa na Jean Ahoua wa Simba akiwa na mabao 7.

kwa Upande wa pasi za mabao Feisal Salum wa Azam FC anaongoza kwa kutoa pasi za mabao tisa akifuatiwa na Jean Ahoua wa Simba na Salum Kihimbwa wa Fountain Gate wote wakiwa na pasi za mabao matano.

Mlinda Mlango wa Simba Moussa Camara anaongoza kwa upande wa hati safi (Clean sheets) akiwa nazo 12 akifuatiwa kwa karibu na Patrick Munthali wa Mashujaa mwenye ‘Clean Sheets’ nane wakifuatiwa na Metacha Mnata wa Singida Black Stars na Djigui Diarra wa Young Africans wenye  ‘Clean sheets’ saba kila mmoja.

Jedwali hapo chini limejumuisha wachezaji wote waliohusika kwenye ufungaji na utengenezaji wa mabao sambamba na walinda milango wote wenye hati safi ‘Clean sheets’.

NBC PREMIER LEAGUE SCORERS

RankPlayerClubPositionGoals
1civJean AhouaSimbaMidfielder16
2tanClement MzizeYoung AfricansForward14
3ghaJonathan SowahSingida BSForward13
4ugaSteven MukwalaSimbaForward13
5cmrLeonel AtebaSimbaForward13
6zimPrince DubeYoung AfricansForward13
7civPacome ZouzouaYoung AfricansMidfielder12
8gamGibril SillahAzamMidfielder11
9kenElvis RupiaSingida BSForward10
10bfaKi Stephane AzizYoung AfricansMidfielder9
11ugaPeter LwasaKagera SugarForward8
12tanNassor SaadunAzamForward8
13tanPaul PeterDodoma JijiForward8
14kenMathew TegisiPamba JijiForward7
15tanOffen ChikolaTRA UnitedForward7
16tanIddi KipagwileDodoma JijiForward7
17tanLusajo MwaikendaAzamDefender6
18codMaxi NzengeliYoung AfricansMidfielder6
19togMarouf TchakeiSingida BSMidfielder6
20tanEdward SongoJKT TanzaniaForward6
21tanWilliam EdgarFountain GateForward6
22zamClatous ChamaYoung AfricansMidfielder6
23codHeritier MakamboTRA UnitedForward6
24tanSelemani MwalimuFountain GateForward6
25tanIbrahim Abdulla BaccaYoung AfricansDefender5
26tanZidane AllyDodoma JijiForward5
27bdiElie MokonoFountain GateForward5
28tanMaabad MaulidCoastal UnionForward5
29tanIddy SelemaniAzamMidfielder5
30tanJoshua IbrahimKenGoldForward5
31tanErasto NyoniNamungoDefender5
32tanJafari KibayaMashujaaForward5
33tanOscar PauloKMCForward5
34tanMishamo DaudiKenGoldMidfielder5
35tanSelemani BwenziKenGoldMidfielder5
36tanFeisal SalumAzamMidfielder4
37codNgoma FabriceSimbaMidfielder4
38tanSalum KihimbwaFountain GateMidfielder4
39tanLucas KikotiCoastal UnionMidfielder4
40bfaYacouba SongneTRA UnitedForward4
41tanBerno NgassaTanzania PrisonsMidfielder4
42tanBakari SelemaniCoastal UnionForward4
43tanShiza KichuyaJKT TanzaniaForward4
44tanHaruni ChanongoTanzania PrisonsMidfielder4
45tanDavid UromiMashujaaForward4
46tanHerbert LukindoKenGoldForward4
47tanRedemtus MussaKMCMidfielder4
48codElie MpanzuSimbaMidfielder4
49tanKibu DenisSimbaMidfielder4
50civJosephat BadaSingida BSMidfielder4
51tanPius BuswitaNamungoMidfielder3
52ghaEmmanuel KeyekehSingida BSMidfielder3
53tanOscar MwajangaTanzania PrisonsForward3
54somIbrahim EliasKMCMidfielder3
55tanRashid ChamboKMCForward3
56tanPascal MsindoAzamDefender3
57tanShomari KapombeSimbaDefender3
58tanSeif KariheMashujaaMidfielder3
59guiAbdoulaye CamaraPamba JijiMidfielder3
60codMwana Kibuta DavidDodoma JijiMidfielder3
61zamKennedy MusondaYoung AfricansForward3
62cgoHernest MalongaSingida BSDefender3
63tanMudathir YahyaYoung AfricansMidfielder3
64tanIsrael MwendaSingida BSDefender3
65kenDuke AbuyaYoung AfricansMidfielder3
66tanEzekia MwashilindiTanzania PrisonsMidfielder2
67codLulihoshi HeritierDodoma JijiDefender2
68mliYoro DiabyAzamDefender2
69codAndy BikokoTRA UnitedDefender, Midfielder2
70tanIdrisa StambuliMashujaaMidfielder2
71ugaMedie KagereNamungoForward2
72zamObrey ChirwaKenGoldForward2
73tanMaulid ShabanCoastal Union2
74tanDickson AmbundoFountain GateMidfielder2
75tanSalehe MasoudPamba JijiForward2
76civSerge PokouSingida BSMidfielder2
77tanCleophace MkandalaKagera SugarMidfielder2
78tanSaid Hamis NdemlaJKT TanzaniaMidfielder2
79tanJohn BoccoJKT TanzaniaForward2
80tanAbdul SuleimanAzamMidfielder2
81tanValentino MashakaSimbaForward2
82kenAbdalla HassanCoastal Union2
83tanDarueshi SalibokoKMCMidfielder2
84tanMohamed BakariJKT TanzaniaMidfielder2
85tanIsmail AllyTanzania PrisonsMidfielder2
86ngaMorice ChukwuSingida BSMidfielder2
87tanSalehe KambengaKagera SugarDefender2
88tanNajim MaguruJKT TanzaniaForward2
89civAnthony Tra BiSingida BSDefender2
90tanHassan HajiMashujaaMidfielder2

NBC PREMIER LEAGUE ASISSTS

RankPlayerClubPositionAssists
1tanFeisal SalumAzamMidfielder13
2codMaxi NzengeliYoung AfricansMidfielder10
3civPacome ZouzouaYoung AfricansMidfielder10
4civJean AhouaSimbaMidfielder9
5zimPrince DubeYoung AfricansForward8
6civJosephat BadaSingida BSMidfielder8
7bfaKi Stephane AzizYoung AfricansMidfielder7
8codElie MpanzuSimbaMidfielder6
9tanSalum KihimbwaFountain GateMidfielder5
10tanIddy SelemaniAzamMidfielder5
11tanClement MzizeYoung AfricansForward5
12tanMudathir YahyaYoung AfricansMidfielder5
13tanZabona MayombyaTanzania PrisonsForward5
14ghaEmmanuel KeyekehSingida BSMidfielder4
15togMarouf TchakeiSingida BSMidfielder4
16cmrLeonel AtebaSimbaForward4
17tanMohamed HusseinSimbaDefender4
18tanAmosi KadikiloFountain GateDefender4
19tanErasto NyoniNamungoDefender4
20codHeritier MakamboTRA UnitedForward4
21tanIddi KipagwileDodoma JijiForward4
22tanLadaki ChasambiSimbaMidfielder4
23tanKibu DenisSimbaMidfielder4
24tanIsmail MgundaMashujaaForward4
25tanLusajo MwaikendaAzamDefender3
26tanSalmin HozaDodoma JijiMidfielder3
27tanSalehe MasoudPamba JijiForward3
28tanLucas KikotiCoastal UnionMidfielder3
29tanAbdul SuleimanAzamMidfielder3
30bfaYacouba SongneTRA UnitedForward3
31ugaSteven MukwalaSimbaForward3
32tanShomari KapombeSimbaDefender3
33tanDatius PeterKagera SugarDefender3
34zamClatous ChamaYoung AfricansMidfielder3
35tanJafari KibayaMashujaaForward3
36civAnde KoffiSingida BSDefender3
37codChadrack BokaYoung AfricansDefender3
38tanShiza KichuyaJKT TanzaniaForward3
39tanNassor SaadunAzamForward3
40swzBanele JR SikhondzeTRA UnitedMidfielder3
41tanRedemtus MussaKMCMidfielder3
42tanAbdalla Said LansoKMCDefender2
43tanPius BuswitaNamungoMidfielder2
44zamJoshua MutaleSimbaMidfielder2
45tanMaulid ShabanCoastal Union2
46kenMathew TegisiPamba JijiForward2
47tanEdward SongoJKT TanzaniaForward2
48tanDarueshi SalibokoKMCMidfielder2
49tanJoseph MahundiKagera SugarMidfielder2
50ngaMorice ChukwuTRA UnitedMidfielder2
51tanKibwana ShomariYoung AfricansDefender2
52ghaSamuel AntwiPamba JijiMidfielder2
53tanPascal MsindoAzamDefender2
54codMwana Kibuta DavidDodoma JijiMidfielder2
55tanDavid KametaSimbaDefender2
56tanOffen ChikolaTRA UnitedForward2
57codJonathan IkangalomboYoung AfricansMidfielder2
58tanAnack MtambiFountain GateDefender2
59gamGibril SillahAzamMidfielder2
60tanSaleh KarabakaSimbaMidfielder2
61tanGeofrey JuliusNamungoMidfielder2
62codNelson MungangaTRA UnitedMidfielder2

NBC PREMIER LEAGUE 2024/2025 CLEAN SHEETS

LIGI KUU NBC KUREJEA WIKIENDI .

Ligi Kuu ya NBC ligi ya nne kwa ubora barani Afrika inarejea wikiendi hii febuari 1 baada ya mapumziko ya takribani mwezi mmoja .

Ligi hiyo itaanza kwa michezo miwili ya viporo vya mzunguko wa 16 ambavyo ni mechi za Yanga dhidi ya Kagera Sugar Februari 1 katika uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam.

Februari 2 Tabora United itakuwa mwenyeji wa Simba katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora katika mchezo uliokuwa umepangiwa tarehe mpya.

Mzunguko wa 17 utaanza rasmi februari tano hadi saba kwa michezo nane itakayochezwa katika viwanja mbalimbali nchini .

Akizungumza kuhusu kurejea kwa Ligi Afisa Habari wa Bodi ya Ligi (TPLB), Karim Boimanda amesema kuwa maandalizi yote yako tayari na kwa upande wa usimamizi Bodi iko tayari, timu, viwanja vimekaguliwa ubora wake viko na upande wa ratiba ilishatoka mapema” Amesema Boimanda na kuongeza kuwa

“Mapumziko ya Ligi yalitokana na uwepo wa michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyochezwa mwanzoni mwa mwezi januari kisiwani Pemba na pia uwepo wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani yaani CHAN ambazo zilipaswa kufanyika februari kabla ya kusogezwa mbele hadi agosti 2 ambapo Tanzania,Kenya na Uganda ni nchi zinazoandaa michuano hiyo”.

STAND YAILIZA KILUVYA,MBUNI YAJIPATA KWA POLISI NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya NBC Championship Mzunguko wa 16 leo imeendelea kwa michezo minne ya mwisho ya mzunguko huo iliyochezwa viwanja mbalimbali nchini  kuanzia majira ya saa nne  asubuhi  na saa kumi jioni.

Bigman waliwakaribisha Mbeya City katika uwanja wa Ilulu mkoani Lindi saa nne asubuhi baada ya mchezo huo kuahirishwa kuchezwa jana kutokana na mvua iliyonyesha mkoani Lindi  na kusababisha uwanja kujaa maji.

Katika mchezo huo Bigman walifanikiwa kuchukua alama 3 kutoka kwa Mbeya City na kufikisha alama 25 katika msimamo wa Ligi hiyo wakiwa nafasi ya saba  baada ya mchezaji wao Francis Kapeta kufunga bao pekee kwa mkwaju wa penati hivyo mchezo kumalizika 1-0.

Mchezo mwingine ulichezwa majira ya saa kumi jioni ambapo timu ya Stand United waliwakaribisha timu ya Kiluvya katika uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

Dakika ya saba ya mchezo huo Stand United walifungua akaunti ya mabao kupitia mchezaji wao Lukas Sendama na dakika kumi baadae Adam Uledi aliongeza bao la pili hivyo kuwafanya Stand United kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Kiluvya walifanikiwa kupata bao dakika ya 66 ya mchezo huo kupitia mchezaji wao Hassan Bundala na dakika ya 82 Sendama alirudi tena nyavuni hivyo kuwafanya Stand United kuchukua alama zote tatu na mchezo kumalizika kwa 3-1, Stand United wamepanda hadi nafasi ya nne wakiwa na alama 32.

Kwa upande wa mechi ya Mbuni dhidi ya  timu ya Polisi Tanzania iliyochezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha mechi ilianza saa kumi alasiri.

Katika mchezo huo Mbuni walifanikiwa kupata bao dakika ya 33 ya mchezo huo kupitia mchezaji Malulu Thomas kabla ya Hassan Rishedy kuongeza bao la pili dakika ya 44 hivyo Mbuni  hivyo matokeo kubaki hivyo hadi mwisho wa mchezo huo  2-0 hivyo kufikisha alama 23 huku wakiwa nafasi ya tisa kakika msimamo.

Timu ya Transit Camp waliwakaribisha  timu ya Biashara United kutoka mkoani Mara kwenye uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi Mkoani Pwani

Katika mchezo huo Biashara United walifanikiwa kubeba alama tatu baada ya mchezaji wao Timotheo Abubakar kufunga bao dakika ya 28 ya mchezo huo ambao ulitamatika  kwa matokeo ya 0-1 hivyo Biashara kufanikiwa kupata alama tatu mhimu wakifikisha alama 4 huku wakiwa wa mwisho katika msimamo wa Ligi hiyo.