Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

SIMBA YATINGA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA.

MWAKILISHI pekee wa Ligi Kuu ya NBC kimataifa timu ya Simba imefanikiwa kutinga fainali baada ya kuiondoa timu ya Stellenbosch kutoka Afrika Kusini kwa matokeo ya jumla kwa bao 1-0.

Simba imelazimisha suluhu ugenini kwenye uwanja wa Moses Mabhida na kufanikiwa kufuzu baada ya faida ya ushindi wa 1-0 iliyopata kwenye mchezo wa nyumbani uliopigwa uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Simba imefanikiwa kutinga fainali hiyo ya kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza kwenye historia huku ikiwa timu ya pili kutoka kwenye Ligi Kuu ya NBC kufuzu fainali hiyo ndani ya miaka mitatu ikiungana na Young Africans iliyofanya hivyo mwaka 2023.

Simba itakutana na RS Berkane ya Morocco kwenye fainali hiyo iliyofuzu baada ya kuifunga CS Constantine ya Algeria kwa ushindi wa jumla kwa mabao 4-1.

Simba itaanzia ugenini Morocco Mei 17 huku mchezo wa pili na wa mwisho katika shindano hilo ukitarajiwa kupigwa Mei 25 kwenye uwanja wa Mkapa, Dar.

VIWANJA NANE ‘KUWAKA MOTO’ LIGI YA NBC CHAMPIONSHIP KESHO

LIGI ya NBC Champioship inaendelea kushika kasi ikielekea mwishoni  na  hapo kesho michezo nane ya mzunguko wa 28 itachezwa katika viwanja mbalimbali nchini majira ya saa kumi jioni .

Timu ya Cosmopolitan ambayo iko nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC itaikaribisha timu ya Stand United iliyopo nafasi ya tatu kwenye msimamo katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Green Warriors iliyopo nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi ya Champioship itaikaribisha timu ya Biashara United ambayo ipo nafasi ya mwisho kwenye msimamo mchezo utakaochezwa uwanja wa Azam Complex Dar es Salaam.

Transit Camp  ikiwa kwenye nafasi  ya 14 katika msimamo itaikaribisha timu  ya TMA  iliyopo nafasi ya tano kwenye msimamo mchezo utakaochezwa katika uwanja wa TFF Centre uliopo Kigamboni mkoani Dar es Salaam.

Timu ya Kiluvya iliyopo nafasi ya 12 itaikaribisha timu ya  Mbuni ambayo iko nafasi ya tisa katika mchezo utakaochezwa uwanja wa Mabatini mkoani Pwani.

Mbeya Kwanza  iliyo nafasi ya sita itachuana  vikali na African Sports iliyo nafasi ya 15 mchezo utakaochezwa uwanja wa Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara.

Timu ya Bigman iliyo nafasi ya saba itawaalika timu ya Mtibwa Sugar inayoongoza Ligi ya Championship ya NBC katika uwanja wa Ilulu mkoani Lindi.

Wachimba madini yaani Geita Gold iliyo nafasi ya nne kwenye msimamo itawakaribisha Mbeya City iliyo nafasi ya pili katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita huku Songea United iliyopo nafasi ya nane ikiwakaribisha Polisi Tanzania iliyo nafasi ta 10  katika uwanja wa Majimaji mkoani Songea.

 

 

MZIZE NI MOTO WA KUOTEA MBALI LIGI KUU YA NBC.

MCHEZAJI wa Young Africans raia wa Tanzania Clement Mzize ameendelea kuwa ‘Mwiba’ kwa mabeki wa timu pinzani baada ya kufanikiwa kufunga jumla ya mabao 13 hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC.

Mzize amefunga idadi hiyo ya mabao huku timu yake ikisalia na michezo minne kutamatika kwa msimu wa 2024/25.

Prince Dube wa Young Africans na Jean Ahoua wa Simba wanafuata nyuma ya Mzize wakifunga mabao 12 kila mmoja huku Ahoua akifunga mikwaju ya penati mitano hadi sasa na kuwa kinara wa kufunga mabao kwa penati.

Jonathan Sowah anafuatia akifunga jumla ya mabao 11 huku akiwa amecheza michezo tisa pekee baada ya kujiunga na timu yake kwenye dirisha dogo la usajili.

Elvis Rupia wa timu ya singida Black Stars anafuata nyuma ya mshambuliaji mwenzake wa timu ya Singida Jonaathan Sowah akiwa na mabao kumi.

MBEYA CITY WAKALI WA MABAO LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC.

JOTO la nani kwenda Ligi Kuu namba nne kwa ubora barani Afrika Ligi Kuu ya NBC linazidi kupanda huku timu ya Mbeya City ikiongoza kwa upande wa kufunga mabao mengi kuliko timu yoyote katika Ligi ya Championship ya NBC.

Mbeya City wamefanikiwa kufunga mabao 55 katika michezo 27 ambayo timu hiyo imecheza huku ikiwa imeruhusu bao 24 na kukusanya alama 59 ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Mtibwa Sugar.

Mtibwa Sugar wanafuatia kwa kufunga mabao ikiwa imefanikiwa kufunga mabao 53 na ikiruhusu mabao 15 katika michezo 27 iliyocheza huku ikiwa imekusanya alama 66 na ikiongoza katika msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.

Stand United na Geita Gold wote wamefanikiwa kufunga mabao 47 kila timu huku Stand ikiruhusu mabao 23 pamoja na kuvuna alama 58 ikiwa nafasi ya tatu katika msimamo na Geita Gold ikiruhusu mabao 21 wote wakiwa  wamecheza michezo 27 katika Ligi hiyo.

Mbeya Kwanza imefanikiwa kufunga mabao 38 baada ya kucheza michezo 27 ikiruhusu nyavu zake kutikiswa mara 24 na ikiwa nafasi  ya sita katika mbio za ubingwa wa Ligi hiyo.

YOUNG AFRICANS YAILIZA FOUNTAIN GATE.

UTAMU wa Ligi  Kuu ya NBC unazidi kukolea ambapo jana katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara  timu ya Fountain Gate iliikaribisha timu ya Young Africans katika mchezo uliochezwa majira ya saa kumi jioni.

Katika mchezo huo timu zote zilianza kucheza kuwa kasi ili kuweza kupata alama tatu muhimu ambapo iliwachukua dakika 38 timu ya Young African kufungua ukurasa wa abao kupitia mshambuliaji wao Clement Mzize huku dakika ya 43 Kiungo wa timu hiyo Aziz Ki akiongezea bao la pili hivyo kuwafanya kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza 0-2.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Fountain Gate wakitafuta nafasi ya kusawazisha ambapo hatahivyo ndoto zao zilizimwa baada ya dakika ya 70 Clement Mzize kuongeza bao la tatu huku Clatous Chama akiweka bao la nne dakika ya 89 hivyo mchezo kutamatika kwa matokeo ya 0-4.

Mchezaji wa Young Africans,Clement Mzize alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mchezo huo.