Author: Loveness Bernard

MTIBWA SUGAR MABINGWA LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC 2024/2025.

TIMU ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/2025.

Mtibwa Sugar kwenye mchezo wake wa mwisho hii Leo dhidi ya Kiluvya iliyochezwa kwenye uwanja wa Manungu Complex imefanikiwa kuibuka na kushinda wa mabao 2-0 myaliyofungwa na Raizin Hafidh dakika ya 36 na 46 ya mchezo huo.

Baada ya ushindi huo Mtibwa Sugar inafikisha alama 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote inayoshiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Mtibwa Sugar ambayo ilishuka daraja kutoka Ligi Kuu ya NBC msimu uliopita imefanikiwa kufunga mabao 58 huku ikifungwa mabao 18 hivyo kujihakikisha nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026.

AHOUA HASHIKIKI, SIMBA IKIWASHA MOTO LIGI KUU YA NBC

UTAMU wa Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika unazidi kukolea timu ya Simba ikiichapa timu ya Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza mabao 5-1.

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa KMC uliopo Mwenge mkoani Dar es Salaam ulishuhudia kiungo wa timu ya Simba Jean Ahoua akifunga Mabao matatu (Hat-Trick).

ilimchukua dakika 16 kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati kabla ya kurejea wavuni tena dakika ya 37 hivyo kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiongoza 2-0 dhidi ya Pamba Jiji.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Ahoua aliongeza bao la tatu hivyo kukamilisha hat-trick dakika ya 48 ya mchezo na mshambuliaji Leonel Ateba aliongeza mabao mawili kwa timu yake ikiwa ni dakika ya 80 na 82 ya mchezo huo huku mchezaji wa Pamba Jiji.

Mathew Momanyi alifunga bao la kufutia machozi kwa timu yake ya Pamba dakika ya 86 hivyo mchezo huo kumalizika 5-1.

Ushindi huo unaifanya timu ya Simba kufikisha alama 66 ikiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku Jean Ahoua akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

HAYA HAPA MABORESHO RATIBA YA LIGI KUU YA NBC

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya maboresho ya ratiba ya Ligi Kuu ya NBC kuanzia mzunguko wa 28 hadi 30 ikiwa ni ratiba ya kukamilisha msimu wa 2024/2025.

Michezo nane ya mzunguko wa 28 inataarajiwa kuchezwa kuanzia mei 12 hadi mei 14 huu timu ya Simba ikicheza dhidi ya Singida Black Stars mei 28 ikiwa ni baada ya mchezo wao wa Fainali ya Kombe la Shirikisho.

Michezo yote nane ya mzunguko wa 29 wa Ligi Kuu ya NBC itachezwa June 18 saa 10:00 alasiri na michezo ya mzunguko wa 30 itapigwa June 22 ambayo itakuwa siku ya kuhitimisha msimu wa 2024/2025.

NGOMA AWALIZA JKT LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja ulioikutanisha timu ya JKT Tanzania na timu ya Simba katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo majira ya saa kumi jioni ulioshuhudia Simba ikishinda kwa bao moja.

Iliwachukua dakika 45 Simba kuandika bao kupitia kwa kiungo wake Fabrice Ngoma baada ya kupokea pasi kutoka kwa mshambuliaji Steven Mukwala na kuifanya Simba kwenda mapumziko ikiwa inaongoza bao moja.

Kipindi cha pili kilianza ambapo JKT Tanzania walijitahidi kulisaka lango la Simba bila kupata bao na hadi mchezo unatamatika ‘Mnyama’ alikuwa mbele kwa bao la Ngoma.

Simba ilifanikiwa kubeba alama zote tatu na kufikisha alama 63 katika michezo 25 iliyocheza huku ikiendelea kusalia katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC

JKT KUWAKARIBISHA SIMBA ISAMUHYO LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC itaendelea kesho kwa mchezo mmoja ambapo timu ya JKT Tanzania itaikaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni mkoani Dar es Salaam  majira ya saa kumi jioni.

Mchezo huo ambao ni mchezo wa mzunguko wa 25 ulishindwa kufanyika hapo awali kutokana na ugumu wa ratiba ya Simba iliyokuwa  na michezo ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

JKT Tanzania ipo nafasi ya saba katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imefanikiwa kufunga mabao 24 na kuruhusu mabao 24 katika michezo 26 ambayo timu hiyo imeshacheza mpaka sasa huku ikikusanya alama 32.

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo  wa Ligi  Kuu ya NBC ikiwa imekusanya alama 60 katika michezo 23 ikifunga mabao 54 na kuruhusu mabao tisa .