Category: STORY

FOUNTAIN, SIMBA ‘KUKIPIGA’ COASTAL KUIKARIBISHA DODOMA JIJI LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo katika mikoa ya Arusha na Tanga ambapo timu ya Fountain Gate itaikaribisha timu ya Simba katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid huku Coastal ikiikabili Dodoma Jiji katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Mchezo wa kwanza utaanza majira ya saa 10:00 jioni kwa Fountain Gate kuikaribisha timu ya Simba, mchezo huo ukiwa muhimu kwa timu hizo ikiwa ni moja ya kufikia malengo waliyojiwekea.

Fountain Gate iko nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 17 ikishinda michezo minne, sare nne na kufungwa michezo tisa huku ikifanikiwa kukusanya alama 16.

Wachezaji wa Simba.

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 17 kushinda michezo 10 sare sita na kufungwa mchezo mmoja huku ikiweza kukusanya alama 36.

 

Kwa upande wa mchezo wa Coastal Union utapigwa majira ya saa kumi na mbili jioni ikiwa ni mchezo wa kimbinu kwani kila timu ikizitaka alama zote tatu muhimu ili kusonga mbele ndani ya malengo waliyojiwekea msimu huu.

Coastal Union iko nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 ushindi tatu, sare saba na kufungwa michezo nane huku ikiweza kukusanya alama 16.

Wachezaji wa Dodoma Jiji.

Dodoma Jiji ipo nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18 ikiwa imeshinda michezo sita, sare sita na kufungwa michezo sita huku ikiwa imekusanya jumla ya alama 24.

VITA YA MABAO YA NJE YA BOKSI INAVYOKWENDA LIGI KUU YA NBC.

 

MSIMU wa Ligi Kuu ya NBC unaendelea huku ushindani wa mabao ya nje ya boksi ukishika kasi na wachezaji wakionyesha uwezo mkubwa wa kupiga mashuti ya mbali na kufunga mabao ya kuvutia.

Kinara wa orodha hiyo ni Ismail Mhesa kutoka Mtibwa Sugar akiwa amefunga mabao matatu nje ya boksi na kuonyesha ubora mkubwa wa kupiga mbali na kuwa tegemeo kwa timu yake akifunga mabao hayo walipokutana na timu za Prisons, Young Africans na TRA.

Sambamba naye ni Iddi Selemani wa Azam ambaye pia ana mabao 3 huku akiendelea kuwa na mchango mkubwa kwa timu yake ya Azam akitumia ubunifu na uwezo wa kufunga akiwa nje ya eneo la hatari na akifanya hivyo mara mbili alipokutana na KMC huku bao moja akiwafunga TRA.

Nafasi ya tatu inashikiliwa na Ibrahim Imoro anayekipiga Singida Black Stars akiwa na mabao matatu ambayo aliyapata walipokutana dhidi ya Prison na Mbeya City huku akinyesha uthabiti mkubwa katika mashuti ya mbali na kuongeza nguvu safu ya ushambuliaji ya timu yake ingawa yeye ni mlinzi.

Wakati huo huo Libase Gueye wa Simba SC ana mabao mawili ya nje boksi akionyesha ubora wake wa kushambulia kwa kutumia nafasi chache anazopata na mabao hayo akiyapata dhidi ya Mashujaa na KMC.

Orodha hiyo inakamilishwa na Kelvin Nashon kutoka KMC mwenye mabao mawili aliyofunga walipokutana na Mbeya City na Singida black star na kumfanya kiungo huyo raia wa Tanzania kuwa tishio kwa timu pinzani.

Kwa ujumla wachezaji wa Ligi Kuu wanazidi kuboresha uwezo wa kufunga mabao ya mbali jambo linaloongeza burudani na ushindani mkubwa ndani ya Ligi.

KMC, PRISONS NANI KUMFUNGA PAKA KENGELE LIGI KUU YA NBC?

LIGI Kuu ya NBC inarejea rasmi leo mkoani Dar es Salaam kwa mchezo mmoja baada ya mapumziko mafupi kwa ajili ya michezo ya Kombe la Shirikisho ambapo timu ya KMC itaikaribisha timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa KMC Complex majira ya saa 1:00 usiku.

Mchezo huo ni muhimu kwa timu zote mbili kwani zinatafuta nafasi ya kubaki katika Ligi Kuu ya NBC kutokana na kuwa nafasi mbaya katika msimamo.

KMC iko nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 18 kwa kushinda michezo miwili, sare mbili na kufungwa michezo 14 huku ikiwa imekusanya alama nane tu.

Prisons ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo 18 kwa kushinda michezo mitatu, sare nne na kupoteza michezo 11 huku ikiwa imekusanya jumla ya alama 13.

TRA KUIVAA SIMBA, MBEYA CITY WENYEJI WA AZAM.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili itakayopigwa kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha ambapo timu ya TRA United itaikaribisha timu ya Simba na kwenyw uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara Mbeya City itaialika timu ya Azam.

Michezo hiyo itakayochezwa saa kumi jioni ni muhimu kwa timu zote kutokana na timu hizo kutaka kujiweka nafasi nzuri ya kupambania ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.

TRA ipo nafasi ya nane katika msimamo ikicheza michezo 17 ushindi sita, sare tano na kufungwa michezo sita huku ikiwa imekusanya alama 23.

Wachezaji wa Simba.

Kwa upande wa Simba iko nafasi ya pili kwenye msimamo ikicheza michezo 16 ushindi mechi 10 sare tano na kufungwa mchezo mmoja huku ikikusanya jumla ya alama 35.

Mchezo wa pili ni muhimu kwa Mbeya City ambapo timu hiyo inatafuta alama iweze kupanda zaidi katika eneo zuri huku Azam ikiwa katika mbio za ubingwa.

wachezaji wa Mbeya city

Mbeya City ipo nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikicheza michezo 17 kushinda michezo minne, sare nne na kufungwa michezo tisa huku ikikusanya alama 16.

Kwa upande wa Azam ipo nafasi ya tatu ikicheza michezo 17 kwa kushinda michezo nane na sare tisa huku ikikusanya alama 33.

IMORO,BARKER WANG’ARA TUZO MACHI

BEKI wa Singida Black Stars, Ibrahim Imoro amechaguliwa kuwa mchezaji Bora wa mwezi Machi wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku Steve Barker wa Simba akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Imoro alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo kwa mwezi huo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao matatu katika michezo mitano ambayo Singida ilicheza na kuisaidia timu yake kupanda kutoka nafasi ya 10 hadi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

 Beki huyo aliwashinda Anicet Oura wa Simba na Lamine Jarjou wa Singida Black Stars alioingia nao fainali katika mchakato wa Tuzo za Mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kocha wa Simba Steve Barker

Kwa upande wa Barker aliyeingia fainali na Pedro Goncalves wa Yanga na David Ouma wa Singida Black Stars, aliiongoza timu yake kushinda michezo miwili na kutoka sare miwili na kupanda kutoka nafasi ya tatu hadi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

Wakati huohuo Meneja wa Uwanja wa Airtel mkoani Singida, Omar Malule, amechaguliwa kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Machi kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

Mchezaji wa Mbuni,Omari Mponda.

Katika hatua nyingine Omari Mponda wa Mbuni amechaguliwa Mchezaji Bora wa Mwezi Machi wa Ligi ya NBC Championship 2025/26, huku Zuberi Katwila wa Geita Gold, akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mponda aliyeingia fainali na Yusuf Mhilu na Maulid Shaaban wote wa Geita Gold alionesha kiwango chenye mwendelezo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao mawili kwa dakika 155 za michezo miwili aliyotumika mwezi huo.

Kocha wa Geita Gold, Zuberi Katwila.

Kwa upande wa Katwila aliyeingia fainali na Leonard Budeba wa Mbuni na Twaha Beimbaya wa B19, aliiwezesha timu yake kushinda michezo yote miwili iliyocheza na kupanda kutoka nafasi ya pili hadi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi.

Pia Kamati ya Tuzo imeteua magoli matatu bora ambayo yatapigiwa kura na mashabiki wa mpira wa miguu nchini, ili kupata Tuzo ya Goli Bora la Mashabiki kwa mwezi Machi.

Magoli hayo ni Prince Dube (Singida v Yanga dakika ya 38), Joseph

Akandwanaho (TRA v Namungo dakika 90+1) na Ibrahim Imoro (Mbeya City v

Singida Black Stars dakika ya 86).