Category: STORY

DODOMA JIJI WAJIPATA JAMHURI

Timu ya Dodoma Jiji imejipata katika uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri baada ya kuhakikisha wanashinda kila mchezo wawapo hapo.

Dodoma ambayo imecheza na timu ya TRA United jana imefanikiwa kushinda michezo minne katika uwanja huo,sare mbili na huku ikipoteza mchezo mmoja tu katika michezo saba ambayo timu hiyo imecheza uwanjani hapo.

Mchezaji wa Dodoma Jiji,Dickson Mhilu

Katika mchezo wa jana ulionza majira ya saa moja usiku Dodoma ilionekana ikizitaka alama zote tatu kutoka kwa TRA kwani timu hiyo ilitawala mchezo ambapo dakika ya 15 ya mchezo huo Faraji Kayanda alifungua ukurasa wa mabao.

TRA nayo ilionekana ikiuta ka mchezo kwa kutaka kusawazisha hata hivyo ndoto yao ilizimwa na mchezaji wa Gadiel Michael ambaye aliongeza bao la pili kwa timu yake hivto kwenda mapumziko Dodoma ikiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilirejea ambapo dakika ya 55 Edgar William alizidi kudidimiza matumaini ya TRA baada ya kuongeza bao la tatu kwa timu yake ambapo mpaka mchezo unatamatika Dodoma iliibuka na ushindi wa 3-0 hivyo timu hiyo ilipanda kutoka nafasi ya saba hadi ya sdita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
[13/02/2026, 09:26:53] Honest Tplb: mkuu

Mahesabu makali Championship

MAHESABU MAKALI NBC CHAMPIONSHIP IKIINGIA MZUNGUKO WA 18.

Mzunguko wa 18 wa NBC Championship unaanza leo ukiwa umebeba presha na mahesabu makali kwa kila timu. Kadri msimu unavyoelekea hatua ya mwisho, kila alama imekuwa ya thamani kubwa katika mbio za kupanda Ligi Kuu ya NBC na vita ya kujiokoa kushuka daraja.

Timu nne zilizo juu ya msimamo Geita Gold, Kagera Sugar, Mbeya Kwanza na Transit Camp zinaingia katika mzunguko huu zikitambua kuwa ushindi pekee ndio utakaozidi kuweka hai ndoto zao za kupanda daraja. Tofauti ya alama kati yao si kubwa, hali inayofanya kila mchezo kuwa wa hadhi ya fainali.

Katika ratiba ya mzunguko huu, Kagera Sugar itaialika Bigman kwenye Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera, huku Transit Camp wakisafiri hadi Songea kuvaana na Songea United katika Uwanja wa Majimaji.
Macho mengi yataelekezwa mkoani Geita ambako Geita Gold watakuwa wenyeji wa Mbeya Kwanza kwenye Uwanja wa Nyankumbu, mchezo unaotajwa kuwa na uzito mkubwa katika kuamua mwelekeo wa kileleni.

Lakini kwa upande wa chini ya msimamo nao si shwari. Timu za B19, Hausung, Barberian na African Sports zinaingia katika michezo ya mzunguko huu zikiwa chini ya presha kubwa ya kutafuta ushindi ili kujinasua kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja na michezo ya mtoano.

Kupoteza alama katika hatua hii kunaweza kuongeza mzigo wa presha na kuifanya mizunguko ijayo kuwa migumu zaidi kwao.

Majibu ya mahesabu makali ya mzunguko wa 18 yatapatikana ndani ya dakika 90 za kila mchezo. Je, ni nani ataongeza kasi ya alama na kujitenga kileleni? Na nani atasalia kuhesabu maumivu ya kupoteza nafasi muhimu?

NBC Championship imeingia katika hatua ambayo makosa madogo yanaweza kugharimu msimu mzima.

COASTAL, PAMBA ZATAMBA LIGI KUU YA NBC.

 

TIMU ya Coastal Union imeonyesha ubabe ugenini katika Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya baada ya kuichapa Tanzania Prisons mabao 4-1. 

Mchezo ulianza kwa kasi Coastal Union wakipata bao la mapema zaidi kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu lililofungwa sekunde ya 58 kupitia kwa Bakari Msimu na dakika tatu kabla ya mchezo kwenda mapumziko Shiza Kichuya aliongeza jingine kwa kichwa akipokea pasi safi kutoka kwa Bakari Msimu. 

Tanzania Prisons haikukata tamaa na kuendelea kushambulia jitihada zilizozaa matunda dakika ya 45+2 kupitia kwa George Mpole aliyewafungia bao lililowapa matumaini kabla ya mapumziko.

Dakika ya 51 Bakari Msimu aliongeza bao lake la pili katika mchezo huo na kuifanya Coatal kuongoza 3-1 kabla ya Cleophace Mkandala kuhitimisha karamu ya mabao kwa kufunga dakika ya 90+5 na kuhitimisha ushindi mnono wa mabao 4-1.

Mchezo mwingine uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza na Pamba Jiji kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Namungo.

Bao pekee la mchezo huo lilifungwa dakika ya 55 kupitia kwa Mathew Tegisi lililodumu hadi mwisho wa dakika 90 na kuwapa Pamba Jiji alama tatu muhimu.

DODOMA YAPANDA NAFASI YA SITA LIGI KUU YA NBC.

 

DODOMA Jiji imeendelea kuonyesha makali yake kwenye Ligi Kuu ya NBC baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2–1 dhidi ya KMC katika mchezo uliochezwa Jijini Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri.

Bao la kwanza la Dodoma Jiji lilifungwa dakika ya 43 na Faraji Kayanda na Kipindi cha kwanza kumalizika Dodoma ikiwa mbele kwa bao moja.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku KMC ikijaribu kusawazisha na jitihada zao zilifanikiwa dakika ya 76 baada ya Rashid Chambo kufunga bao la kusawazisha na kuirejesha timu yake mchezoni.

Hata hivyo iliwachukua dakika moja pekee Dodoma kurejea kwenye uongozi kwa bao la Iddi Kipangwile na kufanya mabao kuwa 2–1 hadi mchezo unamalizika.

Katika mchezo huo, Khleffin Hamdoun alionyesha kiwango cha juu na hatimaye kuchaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mechi akichangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa Dodoma Jiji.

Ushindi huo unaifanya Dodoma Jiji kufikisha alama 17 na kuendelea kushika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi huku KMC ikisalia nafasi ya mwisho (16) ikiwa na alama 8 hali inayozidi kuwaweka kwenye presha ya kusaka matokeo chanya katika michezo ijayo ili kusalia Ligi Kuu ya NBC.

LIGI KUU YA NBC ‘KUCHANJA MBUGA’ LEO.

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili itakayochezwa katika mikoa ya Mwanza kwenye uwanja wa CCM Kirumba na Mbeya kwenye uwanja wa Sokoine.

Mchezo wa kwanza utakuwa saa 8:00 mchana ambapo timu ya Pamba Jiji ya Mwanza itaialika timu ya Coastal Union ya Tanga katika ‘dimba’ la Kirumba.

Pamba Jiji inashika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 12 ikishinda minne, sare tano na kufungwa mitatu huku ikikusanya alama 17.

Coastal ipo nafasi ya 12 katika msimamo ikicheza michezo 12 ikishinda miwili, sare tano na kufungwa michezo mitano huku ikikusanya alama 11.

Mchezo wa pili leo utakuwa majira ya saa 10:15 alasiri ambapo timu ya Tanzania Prisons itaialika timu ya Mashujaa katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.

Prisons ipo nafasi ya 15 ikiwa imekusanya jumla ya alama nane ikiwa imeshinda michezo miwili, sare mbili na kufungwa michezo sita.