Category: STORY

MTIBWA VS GEITA

MTIBWA, GEITA VITA YA UONGOZI NBC CHAMPIONSHIP.

JUMLA ya mechi tano (5) zinachezwa leo Februari 26, 2025 kwenye mikoa ya Lindi, Pwani, Morogoro na Arusha huku michezo yote ikianza saa 10:00 alasiri.

Mchezo unaosubiriwa kwa hamu hii leo unazikutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya Geita Gold kwenye uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, Mtibwa inaongoza msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 48 huku Geita Gold ikishika nafasi ya pili ikiwa na alama 45.

Upekee wa mchezo huu ni kuwa yeyote anayeshinda anakaa kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC, Mchezo wa Duru ya kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita, Geita Gold ilishinda kwa bao 1.

Mkoani Lindi Bigman FC itaialika Biashara United, Cosmopolitan itakuwa mwenyeji wa Kiluvya Jamhuri – Morogoro, kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani Transit Camp itawapokea Green warriors, mchezo wa mwisho kwa leo utazikutanisha Mbuni dhidi ya Mbeya City kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

LADHA ZA LIGI KUU KUCHEZWA VIWANJA VITATU

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa mzunguko wa 22  kuanza kuchezwa  katika viwanja vitatu tofauti nchini kuanzia saa nane mchana.

Mchezo wa kwanza utakaochezwa leo saa nane mchana ni timu ya Fountain Gate itaikaribisha timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara majira ya saa nane mchana.

Fountain Gate ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku  ikiwa imevuna alama 22 na kufunga mabao 25 na kufugwa 39 na Tanzania Prisons ipo nafasi ya 14 ikiwa na alama 18 mabao y kufunga 12 na kufungwa 26.

Singida Black Stars itaikaribisha timu ya Mashujaa katika uwanja wa CCM Liti mkoani Singida mchezo utakaochezwa majira ya saa kumi jioni.

Singida Black Stars ipo nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imefunga mabao 28 na kuruhusu nyavu zao kufungwa mara 19, Mashujaa ipo nafasi ya tisa katika msimamo ikiwa imefunga mabao 17 na kufunwa mabao 23.

Mechi ya mwisho leo itachezwa majira ya saa moja jioni ambapo timu ya Kagera Sugar itaikaribisha timu ya KMC katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Kagera Sugar ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo ikiwa imefunga mabao 16 na kuruhusu mabao 30 huku KMC ikiwa nafasi ya 10 ikiwa na alama 23 na ikifunga mabao 15 na kuruhusu 32.

 

SIMBA VS AZAM

MZIZIMA ‘DERBY’ HAKUNA MBABE.

HAKUNA Mbabe ndivyo unavyoweza kusema baada ya mchezo wa ‘Derby’ ya mzizima kati ya Simba SC na Azam FC kutamatika kwa sare ya mabao 2-2 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mabao ya Azam FC yamefungwa na Gibrill  Sillah na Zidane Sereri huku yale ya Simba SC yakifungwa na Elie Mpanzu na Abdulrazack Hamza.

Zidane Sereri wa Azam FC alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo, Zidane aliyecheza dakika 10 pekee alihusika kwenye bao la mwisho la Azam FC ambalo liliihakikishia Azam FC kupata alama moja kwenye mchezo huo.

Simba inendelea kusalia nafasi ya pili ikiwa na alama 51 baada ya michezo 20 wakati Azam FC ikiwa nafasi ya tatu ikiwa na alama 44 kwenye michezo 21 ya Ligi Kuu ya NBC.

MZIZIMA DERBY

NANI KUIBUKA MBABE WA MZIZIMA ‘DERBY’ LEO ?

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Februari 24, 2025 kwa mchezo mmoja wa ‘Derby’ ya Mzizima kati ya Simba SC na Azam FC kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia majira ya saa 1:00 usiku.

Simba inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na alama 50 baada ya michezo yake 19 huku ikifunga mabao 41 na kuruhusu sita (6) pekee.

Kwa upande wa Azam FC ina jumla ya alama 43 baada ya michezo 20 ya Ligi Kuu ya NBC ikifunga mabao 29 na kuruhusu tisa (9) pekee.

Mara ya mwisho timu hizi zilikutana Septemba 26, 2024 visiwani Zanzibar, na mchezo huo kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kila timu imefanya maboresho kwenye kikosi chake katika dirisha dogo la usajili ambapo Simba imemuongeza kikosini Elie Mpanzu huku Azam FC ikiwasajili Zidane Sereri na Landry Zouzou.

TAARIFA YA KAMATI YA USIMAMIZI WA LIGI YA BODI YA LIGI KUU

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Februari 21, 2025 ilipitia mwenendo na matukio ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Ligi Kuu ya NBC

Mechi Namba 140: Mashujaa FC 0-0 Coastal Union

Klabu ya Mashujaa ya Kigoma imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi kinyume namatakwa ya Kanuni ya 17:21 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo, na kusababisha mdhamini mwenye haki yamatangazo ya runinga, Azam Media Limited kushindwakupata picha za tukio la timu kuwasili. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 147: JKT Tanzania 0-1 Singida BS

Klabu ya Singida BS imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kutokutumia chumba maalumu cha kubadilishia nguo, kinyume na matakwa yaKanuni ya 17:20 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 150: Tabora United 1-1 KenGold

Klabu ya Tabora United imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 2,000,000 (milioni mbili) kwa kosa la wawakilishi watimu hiyo kufika kwenye kikao cha maandilizi ya mchezo bila kifaa chochote kinyume na matakwa ya kanuni ya17:2(2.2) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:(2.2 & 62) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 151: Azam FC 2-0 Mashujaa FC

Klabu ya Mashujaa ya imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuchelewakurejea kiwanjani baada ya muda wa mapumziko kumalizika. Mashujaa walichelewa kutoka vyumbani kwa dakika tano (5) jambo lililosababisha kuchelewa kuanzakwa kipindi cha pili.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:(33 & 62) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mchezaji Seif Karihe wa Mashujaa ameadhibiwa kwa kufungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Azam FC, Feisal Salum. Karihe alimkanyaga Feisal wakati akiwa chini baada ya kumfanyia rafu.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:5 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Mechi Namba 155: Namungo FC 0-3 Simba SC

Mchezaji wa Namungo Daniel Amoah ameadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuonekana akimwaga vimiminika kwenye goli jambolililohusianishwa na vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina.Amoah alionekana akifanya tukio hilo wakati timu ya Simba ikijiandaa kupiga penati.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:3 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

TAARIFA

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabuya kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi aliyoadhibiwa na mwamuzi wa mchezo tajwahapo juu. Kamati imefikia maamuzi hayo baada ya kujiridhisha kuwa maelezo yyaliyopo kwenye ripoti yamwamuzi hayana ushahidi wa kutosha unaoendana namarejeo ya picha mjongeo.

Mechi Namba 157: Mashujaa 2-0 Pamba

Klabu ya Mashujaa ya mkoani Kigoma imeadhibiwa kwakupewa onyo kali kwa kosa la Watoto waokota mipira (ball kids) kuchelewa kwa makusudi kurejesha mipira uwanjanikwa wakati. Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:48 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za mchezo.

Mchezaji wa klabu ya Pamba Jiji ya Mwanza, KassimSuleiman ameadhibiwa kwa kufungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumpiga kwa kutumia mpira ‘Ball Kid’ baada ya kukaa nampira huo muda mrefu bila kuurejesha kiwanjani. Mchezaji huyo aliadhibiwa kwa kadi nyekundu pia na mwamuzi wa mchezo kwa kosa hilo Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 41:5 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Mechi Namba 159: Young Africans 2-1 Singida BS

Klabu ya Young Africans imeadhibiwa kwa kupewa onyo kali kwa kosa la viongozi wake kuingia kwenye eneo la kuchezea (pitch area) baada ya mchezo tajwa hapo juukukamilika.

Viongozi hao wa klabu ya Yanga walioingia uwanjani walisababisha kukosekana kwa utulivu wakati wamahojiano ya mdhamini mwenye haki za matangazo yaruninga.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:50 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 160: KenGold 1-0 Kagera Sugar

Klabu ya KenGold imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la maafisa wake kuchelewa kuwasili kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo (MCM). Maafisa hao walifika kwenye kikao saa 4:30asubuhi badala ya saa 4:00 asubuhi kinyume na matakwaya Kanuni ya 17:2(2.2) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Ligi ya Championship ya NBC

Mechi Namba 151:  Stand United 2-1 TMA

Klabu ya TMA imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuharibu uzio wauwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga. TMA walifanya uharibifu huo ili wachezaji wao wapite chini ya uzio badala ya kupita kwenye mlango rasmi.

TMA walitumia eneo hilo la uzio lililoharibiwa kwa kuingiakiwanjani wakati wa kupasha misuli moto, wakati wakwenda kuanza kwa mchezo, wakati wa mapumziko nabaada ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:21 ya Ligi ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi yaChampionship kuhusu Taratibu za Mchezo.