Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

SIMBA ‘YAIBAMIZA’ KMC LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC Complex, mkoani Dar es Salaam kati ya KMC ikiikaribisha timu ya Simba na kushuhudia ‘Mnyama’ akishinda 1-2 ugenini.

Mchezo huo ulianza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kuwa na ari ya kuzitaka alama tatu muhimu KMC ikitaka kujihakikishia nafasi ya kusalia Ligi Kuu ya NBC msimu ujao huku Simba ikijiimarisha kwenye mbio za ubingwa.

Dakika nane ziliitosha timu ya KMC kufungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Rashid Chambo kabla ya timu ya Simba kusawazika kupitia mshambuliaji wake Steven Mukwala dakika ya 15 ya mchezo na dakika 46 aliongeza bao la pili hivyo mchezo kumalizika kwa 1-2.

Simba imefikisha alama 69 ikiwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikifunga mabao 62 na kuruhusu mabao 11 katika michezo 26 ambayo timu hiyo imecheza huku KMC ikiwa nafasi ya 11 na alama 30 ikifunga mabao 23 na kuruhusu mabao 41 katika michezo 27 ambayo timu hiyo imeshacheza.

AHOUA HASHIKIKI, SIMBA IKIWASHA MOTO LIGI KUU YA NBC

UTAMU wa Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika unazidi kukolea timu ya Simba ikiichapa timu ya Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza mabao 5-1.

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa KMC uliopo Mwenge mkoani Dar es Salaam ulishuhudia kiungo wa timu ya Simba Jean Ahoua akifunga Mabao matatu (Hat-Trick).

ilimchukua dakika 16 kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati kabla ya kurejea wavuni tena dakika ya 37 hivyo kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiongoza 2-0 dhidi ya Pamba Jiji.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Ahoua aliongeza bao la tatu hivyo kukamilisha hat-trick dakika ya 48 ya mchezo na mshambuliaji Leonel Ateba aliongeza mabao mawili kwa timu yake ikiwa ni dakika ya 80 na 82 ya mchezo huo huku mchezaji wa Pamba Jiji.

Mathew Momanyi alifunga bao la kufutia machozi kwa timu yake ya Pamba dakika ya 86 hivyo mchezo huo kumalizika 5-1.

Ushindi huo unaifanya timu ya Simba kufikisha alama 66 ikiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku Jean Ahoua akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

KIVUMBI CHA LIGI KUU YA NBC KUENDELEA LEO.

IKIELEKEA siku za mwisho za msimu wa 2024/25 Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja utakaokutanisha timu ya Simba itakayokuwa uwanja wa nyumbani wa KMC Complex dhidi ya Pamba Jiji kutoka Mwanza.

Simba iliyoshinda mchezo wake uliopita kwa bao moja ugenini dhidi ya JKT Tanzania inarudi uwanjani leo kucheza na Pamba Jiji iliyolazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya Fountain Gate.

Pamba inaingia kwenye mchezo wa leo ikiwa timu namba tatu kwa kushinda michezo michache ikishinda sita, nyuma ya Kagera iliyoshinda mitano na KenGold iliyoshinda mitatu.

Simba inaingia kwenye mchezo wa leo akiwa imepoteza mchezo mmoja pekee huku ikiwa timu iliyoruhusu mabao machache hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC ikifungwa tisa.

NGOMA AWALIZA JKT LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja ulioikutanisha timu ya JKT Tanzania na timu ya Simba katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo majira ya saa kumi jioni ulioshuhudia Simba ikishinda kwa bao moja.

Iliwachukua dakika 45 Simba kuandika bao kupitia kwa kiungo wake Fabrice Ngoma baada ya kupokea pasi kutoka kwa mshambuliaji Steven Mukwala na kuifanya Simba kwenda mapumziko ikiwa inaongoza bao moja.

Kipindi cha pili kilianza ambapo JKT Tanzania walijitahidi kulisaka lango la Simba bila kupata bao na hadi mchezo unatamatika ‘Mnyama’ alikuwa mbele kwa bao la Ngoma.

Simba ilifanikiwa kubeba alama zote tatu na kufikisha alama 63 katika michezo 25 iliyocheza huku ikiendelea kusalia katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC

ISAMUHYO CHANGAMOTO KWA ‘VIGOGO’ LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kutimua vumbi leo Mei 5, kwa mchezo mmoja kati ya JKT Tanzania na Simba utakaopigwa kwenye uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam huku uwanja huo ukiwa sehemu ngumu kupata matokeo ya ushindi kwa timu kubwa za Ligi Kuu ya NBC.

JKT yenye ‘maskani’ yake Mbweni, Dar es Salaam imecheza uwanja wake wa nyumbani dhidi ya Young Africans na Azam bila kupoteza mchezo kwenye msimu huu wa 2024/25.

Michezo yote miwili dhidi ya timu hizo JKT haijaruhusu bao lolote kwani michezo hiyo ilimalizika kwa suluhu huku golikipa wa timu hiyo Yakoub Suleiman akimaliza michezo hiyo kwa kukusanya (hati safi) mbili.

JKT leo itakuwa mwenyeji wa ‘Kigogo’ mwingine wa Ligi Kuu ya NBC aliyefanikiwa kufuzu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika timu ya Simba kwenye uwanja huo wa Meja Jenerali Isamuhyo katika mchezo utakaopigwa saa 10:00 alasiri.