MZUNGUKO wa 16 wa Ligi ya Championship ya NBC unaanza kuchezwa leo Januari 24 kwa michezo mitatu kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.
Mchezo wa kwanza utazikutanisha Mbeya Kwanza dhidi ya Songea United kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara kuanzia saa 10:00 alasiri.
Mchezo wa pili utazikutanisha African Sports dhidi ya Cosmopolitan kwenye uwanja wa TFF Center, Mnyanjani – Tanga kuanzia saa 10 alasiri.
Mkoani Pwani Green Warriors itaikaribisha Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Mabatini mchezo ambao utachezwa kuanzia saa 10:00 alasiri.
Mtibwa Sugar ndio kinara wa Ligi ya Championship ya NBC mpaka sasa ikiwa na alama 38 kwenye michezo 15 ya kwanza huku Biashara United ikiburuza mkia ikiwa na alama moja baada ya michezo 15.