Category: STORY

YOUNG AFRICANS WABABE WA DABI YA DAR

LIGI Kuu ya NBC imeendelea jana ambapo mchezo wa Dabi ya Dar es Salaam ambapo Azam iliwakaribisha Young Africans uliochezwa katika uwanja wa Azam Complex majira ya saa moja usiku.

Mchezo huo ulianza kwa kasi kubwa huku Young Africans wakionekana kushambulia kwa kasi kubwa  huku Azam wakionekana kuzuia kwa kasi ya wapinzani wao.

Ilimchukua dakika 11 tu kiungo wa Young Africans Pacome Zouzoua  kufungua ukurasa wa mabao ambapo aliitanguliza timu yake huku Prince Dube akiongeza bao dakika ya 34 ya mchezo huo  na kufanya timu hiyo kwenda mapumziko wakiwa wako mbele kwa mabao 0-2.

Kipindi cha pili mchezo uliendelea kwa timu zote kusaka mabao ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi na dakika ya 81 beki wa Azam Lusajo Mwaikenda alifungua ukurasa wa mabao kwa timu yake hivyo kufanya mchezo kuwa wa kasi ya kushambuliana zaidi ambapo dakika 90 zilitamatika kwa matokeo ya 1-2.

Mshambuliaji wa Young Africans Prince Dube alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuisaidia timu yake kupata ushindi.

 

AZAM, YANGA NANI KUONDOKA NA ALAMA TATU LEO ?

USIKU wa deni haukawii kukucha ndivyo unavyoweza kusema, baada ya kusuburi wiki, Siku hatimaye yamesalia masaa kuelekea mchezo wa ‘Derby’ ya Dar es Salaam ambapo Azam FC itaialika Young Africans kwenye uwanja wa Azam Complex kuanzia saa 1:00 usiku.

Mara ya mwisho kukutana kwenye Ligi Kuu ya NBC Young Africans ilikubali kichapo cha bao 0-1 likifungwa na Gibril Sillah kwenye uwanja wa Azam Complex.

Young Africans inaingia kwenye mchezo huu ikiwa kinara wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na jumla ya alama 64 kwenye michezo 24 huku Azam FC ikiwa nafasi ya 3 na alama zake 51.

Viingilio vya mchezo huo ni 10,000 kwa mzunguko, 15,000 kwa VIP B na 20,000 kwa VIP A na zinapatikana kupitia wakala yeyote wa N-Card.

PAMBA JIJI YABANWA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

Ligi Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja uliozikutanisha Pamba jiji na Fountain Gate kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza majira ya saa kumi Alasiri.

Kipindi cha kwanza kilianza kwa kasi na dakika ya 22 Mathew Momanyi wa Pamba Jiji alipatia timu yake bao la kwanza kwa mkwaju wa Penati


Dakika ya 61 kipindi cha pili Fountain Gate walifanikiwa kujipatia bao la kusawazisha lililofungwa na Elie Makono na kufanya matokeo kuwa 1-1 na dakika za nyongeza Pamba ilipata mkwaju wa penati na kukoswa na Mathew Momanyi aliyepiga na mpira kugonga mwamba hivyo kufanya mchezo kumalizika kwa matokeo ya 1-1.

Matokeo hayo yanaifanya Pamba jiji kushika nafasi ya 10 na alama 27 huku Fountain Gate ikiwa nafasi ya  8 na alama 29 kibindoni.

PACOME AIBEBA YANGA IKIIFUNGA COASTAL LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC Complex ambapo timu ya  Young Africans iliikaribisha timu ya Coastal Union  kutoka Tanga.

Mchezo huo ulianza majira ya saa kumi na robo jioni ambapo timu zote zilikuwa zikishambuliana huku pia zikiimarisha ulinzi katika lango lao ili kutokuruhusu bao lolote.

Ilimchukua dakika 34 mchezaji wa Young Africans Pacome Zouzoua kufungua ukurasa wa mabao hivyo kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao moja.

Kipindi cha pili kilianza ambapo timu zote zilionekana zikitaka alama  tatu  muhimu ambapo hata hivyo mchezo  ulitamatika kwa Young Africans kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Youn Africans imezidi kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa baada ya kufikisha alama 64 huku wakiwa wamecheza michezo 24  na wakiendelea kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu  huku timu ya  Coastal Union ipo nafasi ya13  katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 25.

 

 

 

GUNNERS MABINGWA WA FIRST LEAGUE 2024/2025

TIMU ya Gunners kutoka mkoani Dodoma imefanikiwa kuwa Bingwa wa First League msimu wa 2024/2025 baada ya kuifunga Hausung mabao 3-0 kwenye mchezo wa Fainali uliochezwa jana Azam Complex, Dar es salaam.

Gunners ilimaliza kinara wa Kundi B ikiwa na alama 35 kwenye michezo 14 hivyo kupata nafasi ya kucheza mchezo wa Fainali ulioipa timu hiyo ubingwa.

Kwa upande wa Hausung ilimaliza kinara wa kundi A ikiwa na alama 25 kwenye michezo 14, alama ambazo ziliipa timu hiyo nafasi ya kucheza mchezo huo wa fainali kumtafuta bingwa wa jumla wa First League 2024/2025.

Timu zote mbili zimekata tiketi ya kushiriki Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/2025 baada ya kumaliza vinara wa makundi yao.